
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakati wa hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakati wa hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (kulia) akimpatia mpira mmoja wa wawakilishi wa wachezaji wa timu za mpira kwa ajili ya mashindano ya ligi Samia Cup yanayotarajiwa kufanyika katika Kata ya Chipogolo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyevaa miwani) akisalimiana na baadhi ya wananchi wa Kata ya Chipogolo wakati alipowasili kwa ajili ya hafla ya kugawa vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa hafla ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (aliyeshika mpira) akiteta jambo na Mwenyekiti wa CCM Chipogolo, Bw. Msafiri Mgonela (wa kwanza kulia) wakati wa hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (wa tatu kutoka kulia) akifurahia jambo wakati wa hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup. Kulia kwake ni Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na mmoja wa wawakilishi wa timu ya mpira ya wanawake wakati wa hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Wananchi wa Kijiji cha Chipogolo, Kata ya Chipogolo wakimsikiliza Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene (hayupo pichani) wakati wa hafla ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora na Mbunge wa Jimbo la Kibakwe, Mhe. George Simbachawene akifurahia jambo na mwananchi wa Kata ya Chipogolo aliyehudhuria hafla ya ugawaji vifaa vya michezo ya mashindano ya ligi Samia Cup.
Na. Mwandishi Wetu-Chipogolo
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Kibakwe ameunga mkono mashindano ya ligi Samia Cup na kugawa vifaa vya michezo huku akiahidi kutoa zawadi kwa mshindi wa kwanza kiasi cha fedha shilingi 500,000/=, mshindi wa pili 250,000/= na mshindi wa tatu 150,000/= kuelekea mashindano ya ligi Samia Cup yanayotarajiwa kufanyika katika Halmashauri ya Wilaya ya Mpwapwa, Kata Chipogolo.
Mhe. Simbachawene ameunga mkono mashindano hayo alipokuwa mgeni rasmi kwenye hafla maalum iliyolenga kugawa vifaa hivyo vilivyonunuliwa na Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika.
Mhe. Diwani ninakupongeza sana, kwenye baadhi ya maeneo mimi ndiye ninayeombwa kutoa vifaa vya michezo, lakini leo ni tofauti na nilivyozoea nimekuja kugawa vifaa hivi vilivyonunuliwa nawe, hongera kwa kujitolea na huo ndio uongozi, nami nitaongeza fedha kuanzia mshindi wa kwanza hadi wa tatu. Amesema Waziri Simbachawene.
Akizungumza na wananchi katika Kijiji cha Chipogolo, Waziri Simbachawene ametoa pongezi kwa Mhe. Diwani Kayanda kwa kutoa vifaa hivyo na kutumia fursa ya Mashindano ya Ligi Samia Cup kuwafahamisha wananchi maendeleo ambayo yamefanyika katika kipindi cha miaka mitano chini ya Uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ikiwemo kujengwa kwa vituo vya afya, usambazaji wa umeme, kutatua changamoto ya maji na miundombinu ikiwemo ujenzi wa Barabara kwenye baadhi ya maeneo.
Aidha, Waziri Simbachawene amesema michezo inatoa ajira, inaimarisha afya, inajenga undugu na inaleta furaha kwa jamii hivyo ni vema wananchi wa Chipogolo wakashiriki kwa wingi.
Kwa upande wake Diwani wa Kata ya Chipogolo, Mhe. Kayanda Mwanika amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kukubali kuwa mgeni rasmi na kugawa vifaa hivyo vya michezo na kuunga mkono mashindano hayo kwa kutoa fedha kwa washindi.
Vilevile, Mhe. Kayanda amemshukuru Waziri Simbachawene kwa kushughulikia masuala mbalimbali ya maendeleo katika Kata ya Chipogolo.
Post A Comment: