Taasisi ya Utafiti wa Wanyamapori Tanzania (TAWIRI) ni miongoni kwa washiriki wa Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani (Mei Mosi) Mkoani Arushs inayofanyika Mei 1, 2025, katika Uwanja wa Sheikh Amri Abeid.
Aidha, watumishi wa TAWIRI wameonesha umahiri wao kupitia maandamano ya miguu na pia kupitia gari la maonesho, ambalo lilikuwa moja ya vivutio vikubwa katika maandamno haya, ilikuwa ni fursa kubwa kwa wafanyakazi wa TAWIRI kunadi mchango wa taasisi katika uhifadhi wanyamapori nchini .
Kupitia machapisho, vipeperushi, video na sanamu za wanyamapori, TAWIRI ilidhhirisha mbele ya mgeni rasmi na umma wa Arusha namna tafiti zake zinavyosaidia kuelimisha na kutatua changamoto za uhifadhi ili kuwezesha maendeleo endelevu ya sekta ya utalii, na maisha bora ya Jamie.
Kitaifa, maadhimisho ya Mei Mosi, 2025 yanafanyika mkoani Singida, ambapo Mgeni Rasmi ni Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Post A Comment: