Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Serera,akizungumza wakati akifungua Kongamano la Afreximbank Roadshow lililoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam.

.....

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt Suleiman Serera ameishauri sekta binafsi ya Tanzania kuhakikisha inatumia fursa ya uwepo wa Benki ya Kanda ya Afrika ya Afrexim kupata mitaji itakayowezesha kuongeza thamani mazao na bidhaa za viwandani kwa kiwango cha kimataifa ili kuiwezesha nchi kushindana ndani ya soko la Afrika

Dkt. Serera ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati akiongea na Waandishi wa Habari baada ya kufungua Kongamano la Afreximbank Roadshow lililoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania pamoja na Benki hiyo likilenga kutambua changamoto za wafanyabiashara ili benki hiyo iweze kuzitatua kupitia fursa za mitaji, fursa za masoko na teknolojia

Aidha, Dkt. Serera aliwahimiza Wajasiliamali wa Tanzania, Wawekezaji wa viwanda, na biashara zinazoongozwa na vijana kushirikiana na Afreximbank na kutumia fedha zinazopatikana kwa usindikaji wa kilimo, maendeleo ya mauzo ya nje, ujenzi wa viwanda vya kijani, na biashara ya kikanda.

"Tuwekeze Dodoma, Mbeya, na Kigoma," alihimiza. "Tujenge Maeneo ya Usindikaji wa Mauzo ya Nje, tuimarishe korido za vifaa, na tujenge miundombinu ya kidijitali kwa mfumo wa biashara unaostawi."

Kwa upande wake Rais wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Bw. Vincent Minja amesema jukwaa hilo ni muhimu katika uwezeshaji wa biashara barani Afrika akiweka bayana kuwa biashara kati ya nchi za Afrika bado ni kidogo ikilinganishwa na biashara kati ya nchi za Bara hilo na mabara mengine duniani

Naye Mkurugenzi Mkuu wa Uhusiano wa Wateja wa benki hiyo Bw. Eric Monchu ameihakikishia sekta binafsi ya Tanzania kuwa wako tayari kukuza uchumi endelevu wa Tanzania

Aidha Bw Monchu amebainisha kuwa hadi sasa, Benki hiyo imetoa takriban dola bilioni 2 kuwezesha utekelezaji wa Miradi ya Kimkakati nchini ikiwemo Dola milioni 800 kwa kwa ajili ya Mradi wa Umeme wa Maji wa Julius Nyerere, Dola milioni 290 kwa Reli ya Kati (SGR), Dola milioni 200 kwa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) pamoja na Nyongeza ya fedha kwa benki za ndani na wadau wa sekta binafsi

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) Bi Lulu Mkude amewaalika wadau na mabenki mbalimbali waliohudhuria kongamano hilo kushiriki Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es salaam yatakayoanza tarehe 28 Juni hadi 13 Julai 2025 kwani ni jukwaa zuri la kutangaza biashara na huduma wanazotoa.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Serera,akizungumza wakati akifungua Kongamano la Afreximbank Roadshow lililoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam.

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Serera (katikati ) akizungumza na Viongozi mbalimbali wakiwemo Kaimu Mkurugenzi wa Uhusiano wa wa Wawateja wa Areximbank Bw. Eric Monchu Intong, Rais wa Chemba ya Biashara, Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) Bw. Vincent Minja na Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Bi lulu Mkude kabla ya ufunguzi wa Kowngamano la Afreximbank Roadshow lililofanyika Mei 2025 jijini Dar es Salaam

Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda na Biashara Dkt. Suleiman Serera,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kufungua Kongamano la Afreximbank Roadshow lililoandaliwa na Benki Kuu ya Tanzania lililofanyika jijini Dar es Salaam.

Share To:

Post A Comment: