Kamisaa wa Sensa na Spika Mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Anne Semamba Makinda, ametoa rai kwa wananchi kuanzia ngazi ya chini kutumia takwimu sahihi zilizopatikana kutokana na Sensa iliyofanyika katika shughuli mbalimbali za Maendeleo.

Mhe. Makinda ametoa rai hiyo alipotembelea Banda la Wizara ya Fedha katika Maonesho ya 48 ya Biashara ya Kimataifa (Sabasaba) yanayofanyika katika viwanja vya Julius Nyerere Barabara ya Kilwa, Temeke, jijini Dar es Salaam, ambapo amesisitiza matumizi ya Takwimu sahihi kwa maendeleo.

Amesema Takwimu zilizotokana na sensa zina kila kitu hivyo ni vyema zikatumika kikamilifu katika mipango ya maendeleo lakini pia kutumiwa na watafiti wakiwemo wa vyuo mbalimbali katika kupata majibu ya changamoto mbalimbali zinazoikabili jamii.

Amewataka wananchi kutembelea Banda la Wizara ya Fedha ili kupata elimu ya zianda kuhusu Sensa na takwimu kwa kuwa sasa Ofisi ya Takwimu inafanyakazi ya kutoa elimu kwa umma kuhusu matokeo ya Sensa iliyofanyika.

Share To:

Post A Comment: