Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga amesema Jimbo la Mbulu Mjini lina Vijiji 34 ambapo  Vijiji 31 kati ya hivyo  vimepata umeme.

Ameeleza  hayo bungeni jijini Dodoma ambapo amesema uwa kwa Vijiji vilivyosalia utekelezaji wa miradi unaendelea na kazi itakamilika tarehe 30 Juni 2024.

Ameongeza kuwa, Jimbo la Mbulu Mjini lina mitaa 58 ambapo mitaa 46 ina umeme na mitaa 12 ambayo imesalia itapatiwa umeme kupitia mradi wa kupeleka umeme vitongojini ambao utaanza mwaka wa fedha 2024/2025.

Share To:

Post A Comment: