Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule amesema kuwa Mkoa wa Dodoma una zaidi ya Mizinga ya nyuki 18,000 yenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya kilo 135,000 za asali ambapo kiwango hicho bado ni kidogo ukilinganisha na fursa za ufugaji nyuki zilizopo katila mkoa huu ambapo zaidi ya hekta 1,938,193.za misitu zimehifadhiwa na zinaweza kutumika katika shughuli za ufugaji nyuki.


Senyamule ameeleza hayo mapema leo hii Jijini Dodoma katika ufunguzi wa maonesho ya siku ya nyuki Duniani ambayo kitaifa yanafanyika Jijini hapa iliyobeba kauli mbiu inayosema:NYUKI KWA AFYA NA MAENDELEO,TUWATUNZE.#APIMONDIA 2027 TANZANIA IPO TAYARI.

Na kuongeza kuwa rasilimali zilizopo katika Mkoa wa Dodoma endapo zikarumika vizuri zinaweza kuzalisha zaidi ya kilo milioni 7,000,000. za asali na kuongeza kipato cha kaya pamoja na Taifa.

"Mkoa wa Dodoma una zaidi ya mizinga 18,000 ya nyuki yenye uwezo wa kuzalisha zaidi ya kilo 135,000 za asali. Aidha, kiwango hiki bado ni kidogo ikilinganishwa na fursa za ufugaji nyuki tulizonazo kwenye mkoa wetu ambapo zaidi ya hekta milioni 1,038,193 za misitu imehifadhiwa na zinaweza kutumika kwenye shughuli za ufugaji nyuki. Pia, shughuli za ufugaji nyuki zinaweza kufanyika katika maeneo ya kilimo na kuongeza uzalishaji wa mazao ya kilimo kupitia huduma ya uchavushaji".

"Ndugu Wananchi, Rasilimali zilizopo kwenye mkoa wetu endapo zikitumika vizuri tunaweza kuzalisha zaidi ya kilo milioni 7,000,000 za asali na kuongeza kipato cha kaya pamoja na taifa".

"Hivyo, nitoe rai kwa wananchi wa mkoa wa Dodoma kuchangamkia fursa hii na kufanya shughuli za ufugaji nyuki ili kujiongezea kipato".

Aidha amesema tunapojivunia sekta hii ya nyuki katika Mkoa wa Dodoma lakini hakuna budi kutafakari uendelevu wa sekta hii kwa Mkoa na Taifa kwa ujmla ambapo zipo changamoto zinazoikabili sekta hii ikiwemo matumizi ya dawa za kuua wadudu kwenye kilimo na uchomaji moto misitu ndizo zinazotishia uendelevu wa sekta hii.

"Ndugu Wananchi;Tunapojivunia maendeleo ya sekta ya nyuki katika Mkoa wetu hatuna budi kutafakari kuhusu uendelevu wa sekta hii Mkoani hapa na Taifa kwa ujumla. Sekta ya nyuki inakabiliwa na changamoto ambazo zinatishia uendelevu wake na hivyo kuhatarisha upatikanaji wa mazao ya nyuki kwa siku zijazo. Miongoni mwa changamoto zinazotishia ukuaji wa sekta hii ni pamoja na: matumizi ya dawa za kuua wadudu kwenye kilimo, uchomaji moto misitu, kubadilisha maeneo ya ardhi ya misitu kwa matumizi mengine, kuongezeka kwa kasi ya mabadiliko ya tabia nchi ambayo yanaambatana na mabadiliko ya hewa na mazingira rafiki kwa nyuki kuzalisha mazao yao".

"Pamoja na changamoto zilizopo katika sekta ya nyuki, Mkoa wetu bado una nafasi kubwa ya kukuza na kuendeleza sekta hii. Ni wazi kuwa Mkoa wa Dodoma na Mikoa mingine bado tuna nafasi ya kuhifadhi misitu katika ardhi za Vijiji, misitu ya Halmashauri, misitu ya Serikali kuu na hifadhi za wanyamapori. Hatuna njia ya mkato ambayo itawezesha uendelevu wa mazao ya nyuki sambamba na huduma za mdudu nyuki kwenye mimea zaidi ya kumlinda na kuhifadhi mazingira yake. Niwatake wananchi wa Mkoa wa Dodoma na washiriki wa maadhimisho haya kutumia maonesho ya wadau wa sekta ya nyuki kama jukwaa muhimu la kujifunza na kukuza sekta hii kwa ajili ya kukuza uchumi wa mwananchi mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla".

Awali akitoa salamu za Wizara ya Maliasi na Utali kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara Deusdedit Boyo ambaye ni Mkurugenzi wa Idara ya Misitu na Nyuki iliyochini ya Wizara ya Maliasili na Utalii amesema kuwa Takwimu zinaonesha kuwa tuna aina mbalimbalo za nyuki zipatazo elfu 20 na pia takwimu zinaonesha kwamba karibia asilimia 90 ya mimea you duniani yenye maua inategemea nyuki.

Na kuongezea kuwa sote tu mashahidi na ni ukweli usiopingika juu ya manufaa tunayoyapata kutoka kwa nyuki iwe ni kwa kujua au kuto kujua ila tunapata manufaa ya kipekee sana.

"Takwimu zinaonesha kwamba tuna zaidi ya nyuki wapatao elfu 20 wa aina mbalimbali,pia Takwimu zinaonesha kwamba karibia asilimia 90 ya mimea yote duniani yenye maua inategemea nyuki, Takwimu zinatuonesha kwamba kadiri ya asilimia 75 ya mazao yote ya chakula yanategemea nyuki,I a maana bila nyuki tusingekuwa na mazao ya namna hii".

"Sote tu mashahidi na ni ukweli usiopingika juu ya manufaa mengi tunayoyapata kutoka kwa mdudu nyuki iwe kwa kujua ama kwa kutokujua tumenufaika kwa namna ya kipekee na mazao yao mbalimbali yanayozalishwa na nyuki".

Kilele cha maonesho haya ya siku ya Nyuki Duniani itakuwa ni May 20,2024, ambapo inafanyika Dodoma na Mgeni Rasmi anatarajiwa kuwa Makamu wa Raisi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania p Dkt Philip Mpango.






Share To:

Post A Comment: