Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Bajeti imeridhishwa na usimamizi wa fedha ujenzi wa miradi ya Umwagiliaji katika mashamba ya Taasisi ya Utafiti wa Mbegu (TARI) pamoja na Mashamba ya Wakala wa Mbegu za kilimo (ASA) ikiwemo shamba la mbegu Ngaramtoni pamoja na shamba la mbogamboga Tengeru mkoani Arusha.

Akizungumza na waandishi wa habari, Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mhe. Daniel Sillo (Mb) amesema wajumbe wa Kamati hiyo wameridhishwa na miradi waliyo tembelea ambapo wamesema kuwa miradi hiyo ilitengewa fedha na serikali na kamati hiyo ndio iliyosimamia utengaji wa fedha hizo hivyo kuna kila sababu ya kamati kukagua nakuona thamani ya fedha ilivyotumika katika sekta ya Umwagiliaji.

Amesema miradi hiyo kwa Shamba la Arusha yenye thamani ya Billion 4.4 ikikamilika itaongeza upatikanaji wa Mbegu bora za kilimo Kwa wananchi na kupunguza uaigizaji wa Mbegu kutoka Nchi za nje.

Mwenyekiti Sillo amesema katika sekta ya kilimo Kamati hiyo inamatumaini makubwa ya kupata matokeo chanya ya ukamilishaji wa miradi nakuona matokeo chanya katika Mirada hiyo.

Amesema mpaka sasa Kamati hiyo haina mashaka ya matumizi ya fedha za umma kutokana na kuonekana kwa thamani ya fedha ilivyo tumika.

Aidha ameipongeza Kampuni inayojenga miundombinu hiyo ya Umwagiliaji Pro Agro Global ltd kwa kufanya kazi Kwa uzalendo na kuonesha kuwa vijana wakipewa kazi wanaweza.



Share To:

Post A Comment: