Waziri wa Madini Anthony Mavunde (Kushoto), akisikiliza maelezo kutoka kwa Afisa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Msimamizi Mkuu wa Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini, Bi. Samirah Mohamed (kulia), kuhusu Kliniki ya Biashara inayoratibiwa na Taasisi hiyo, kwenye Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika kwenye viwanja vya EPZ Bombambili Mkoani Geita, leo Septemba 29,2023.

TANTRADE imeshiriki Maonesho hayo ikisimamia Kliniki ya Biashara yenye jukumu la kutoa huduma kwa pamoja kusikiliza na kutatua changamoto za wadau na wananchi mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara.

Afisa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Msimamizi Mkuu wa Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini, Bi. Samirah Mohamed (kulia), na Bi. Clara Mwamba (Kushoto), Afisa Biashara kutoka katika Taasisi hiyo, , wakiwa katika picha ya pamoja kwenye Banda lao inapofanyika Kliniki ya Biashara kwenye Maonesho ya sita ya Teknolojia ya Madini Mkoani Geita.

Afisa Biashara wa Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TANTRADE), na Msimamizi Mkuu wa Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya sita ya Teknolojia Katika Dekta ya Madini Bi. Samirah Mohamed (wa kwanza kulia), akiwa katika picha ya pamoja na watumishi wa Taasisi wezeshi za Serikali zilizoshiriki kwenye Kliniki hiyo katika Maonesho hayo, Geita.

Muonekano wa Banda ya Kliniki ya Biashara katika Maonesho ya Madini Geita.

Share To:

Post A Comment: