DENIS CHAMBI, TANGA.

WAZIRI wa Afya na mbunge wa jimbo la  Tanga mjini Ummy Mwalimu amesema kuwa amejiapanga  kulitangaza jiji hilo kupitia mazao yatokanayo na Bahari na  kuzidi kuwavutia wawekezaji  ambao watasaidia kukuza uchumi wa wananchi na hatimaye  kuchangia pato la Taifa kwa ujumla.

Ummy amesema hayo  leo July 17  katika ziara yake ya kutembelea miradi mbalimbali iliyopo chini ya taasisi Tanga yetu ambayo inafadhiliwa na Botner foundation  ambao wamewekeza jumla ya shilingi Billion 7 kwa awamu ya kwanza  katika sekta ya uvuvi hususani kilimo cha  Mwani,  kunenepesha kaa, kuwawezesha vijana kiuchumi.

"Kwa  niaba ya wakazi wa jiji la Tanga tunapenda kuwashukuru na kuwapongeza sana kwa kuunga mkono jitihada za serikali kuboresha miundombinu kwa wakazi wa jiji la Tanga hususani kufungua fursa mbalimbali za kiuchumi katika miradi ya uvuvi, kuwawezesha  vijana katika kilimo, ufugaji wa kuku na samaki pamoja na kuboresha eneo la Bustani ya Forodhani haya ndio maendeleo ambayo tunataka kuyaona katika jiji letu la Tanga"

"Tunataka kuufanya mwambao wa Tanga kuwa ndio kinara cha uzalishaji  wa  mazao ya Bahari hususani mazao ya Mwani, Majongoo Bahari pamoja na Kaa tunachotaka sasa hivi ni kutafuta wadau wengi zaidi watusaidie kuwekeza  zaidi" alisema Ummy

Amesema  kuwa ataendelea kudumisha mahusiano  na wadau mbalimbali chini ya  wizara  ya mifugo na uvuvi  ili kuendeleaza  mazao yatokanayo na Bahari huku akiwavutia wawekezaji wengi zaidi kuja kuwekeza kwa lengo la kuendelea kutangaza Tanga.

"Nawashukuru sana Botner foundation kwa juhudi wanazoendelea kufanya na kuunga mkono lakini tunahitaji kuboresha ubia zaidi kwaajili ya kuboresha maisha ya wakazi wa jiji la Tanga, kwa kweli tunapaswa kulikumbatia zao la Mwani  ni zao lenye faida kubwa  tutashirikiana na Botner foundation chini ya wizara ya mifugo na uvuvi kuhakikisha tunaendeleza kilimo Cha zao la Mwani kwanza kabisa kuwapa elimu na ujuzi wananchi". alisema Ummy.

Akizungumza mwakilishi wa shirika la Botner foundation Dkt Hassan Mshinda  amesema kwa awamu hii ya kwanza wamefadhili miradi mbalimbali inayotekelzwa ndani ya jiji la Tanga ikiwa na zaidi ya  shilingi Billion 7.

"Tunashukuru sana kwa ushirikiano tunaoendelea kuupata kutoka kwa halmashauri ya jiji na  mbunge wetu Ummy Mwalimu , hii ni kazi iliyofanywa kwa muda wa miaka miwili na nusu lakini  tunategemea kwamba tutaweza kuendelea kwa muda mwingi zaidi na miradi mingine mingi ambayo inalenga kuwasaidia zaidi vijana kuwewezesha kiuvumi" alisema Dkt. Mshinda. 

Kwa upande wake  Afisa uvuvi ambaye ni msimamizi wa mradi wa  uvuvi kupitia  miradi  ya  Tanga yetu Omari Mohammed amesema kuwa kumekuwa na mabadiliko chanya kwa wananchi wanotekeleza   miradi hiyo ambayo imekuwa ikiwaapia  kipato ikiwemo unenepeshaji wa kaa, kilimo cha Mwani,  ufugaji wa samaki wa   sato.

Wakizungumza katika ziara hiyo baadhi ya wavuvi akiwemo Khatibu Enzi  wameeleza changamoto ya  uvuvi haram sambamba na kuibiwa vifaa vyao ikiwemo ngalawa na kuchomewa boti  wakiiomba serikali kuwasaidia kuimarisha ulinzi na usalama na kufanya doria za mara kwa mara .

"Ndani ya miezi mitatu sasa  vyombo vyetu Kama tisa vimepotea  na hii hali imekuwa ukitokea kama doria lakini doria hiyo haina taarifa  kwenye serikali za mitaa au ofisi za mazingira kwahiyo vyombo vikipotea tukivitaguta havijulikani  vikowapi hiyo imekuwa Ni changamoto kubwa sana kwetu sisi wavuvi" alisema Enzi.

Share To:

Post A Comment: