DENIS CHAMBI, TANGA.
Katika kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika halmashauri ya jiji la Tanga imetoa msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula kwenye vituo vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ambapo katika kituo cha Nyumba ya furaha imetoa kilo 20 za mchele, kilo 40 za Maharage na vyandarua 10 wakivipatia vituo 6 vilivyopo hii ikiwa ni njia ya kuonyesha kuwajali na kuwathamini watoto hao.
Akizungumza
katika kituo hicho katibu tawala wilaya ya Tanga Dalmia Mikaya
amewataka wazazi , walezi na jamii kwa ujumla kusimamia majukumu yao
ipasavyo kwa watoto wakiwalinda na athari mbalimbali ikiwemo ukatili
pamoja na matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.
Alisema
kutokana na mabadiliko ya kidigital Dunia imebadilika sambamba na
matukio mengi ya kiukatili dhidi ya watoto yakishamiri hivyo wazazi,
walezi na jamii kwa ujumla wana jukumu kubwa la kuhakikisha wanakiandaa
kizazi ambacho kitakuwa ni tegemeo la kesho.
"Wazazi
walezi tunapaswa kujua kwamba mtoto naye ana haki yake, ikiwemo
kusikilizwa, kulindwa na kuangaliwa kwa umakini niwaombe sana wazazi,
walezi na jamii kwa ujumla kuzingatia usalama wa mtoto hakikisheni
mnasimamia maadili ya mtoto kuanzia nyumbani, na sisi tunatamani tuwe na
Taifa lenye vijana waadilifu baadaye ambao watalisongeza taifa letu
mbele linaendelea ya kiuchumi"
"Kuna
mambo sasa hivi yanayoendelea katika jamii ni mengi dunia
imeahabadilika tupo kwenye mfumo wa kidigital kuna mambo mengi
yanafanyika wakati huu ikiwemo ukatili kwa watoto ,unyanyasaji ,
ubakaji, matumizi mabaya ya mitandao kuna Uhuru mkubwa sana upo kwa
watoto, alisema Mikaya.
Mkuu
wa idara ya maendeleo ya jamii wa jiji la Tanga Simon Mdende alisema
bado hali ya unyanyasaji kwa watoto katika jamii sii shwari licha ya
elimu wanayoendelea kutoa katika jamii kwa mslahi ya mtoto huku
akiwataka wahisani mbalimbali kujitokeza kuvisaidia vituo vinavyolea
watoto ili waweze kupata malezi na huduma bora wanazostahili.
"Katika
halmashauri ya jiji la Tanga kwa watoto wanaoishi kwenye halmashauri ya
jiji la Tanga hali sii nzuri sana kwasababu watoto wanaoishi kwenye
mazingira magumu wamechukuliwa kutoka sehemu tofauti tofauti wengi
tunapowatoa kwenye mazingira waliyozoea wanaathirika kisaikolojia,
katika hivi vituo wanapoishi Hawa watoto bado uchumi sio mzuri sana
kwahiyo jamii inahitajika sana kujitoa na kusaidia hawa watoto ili
kupata huduma mbalimbali" alisema Mdende.
Kwa
upande wake Afisa ustawi wa jiji la Tanga Deogratias Casmiri amewataka
wazazi na walezi pamoja na majukumu mengine kukaa karibu na watoto
kubaini changamoto zinazowakabili katika mazingira ya nyumbani na
mashuleni na hatimaye kuzitatua mapema kabla hawajaathirika kwa namna
yeyote ile ili kuwa na kizazi bora Cha baadaye.
"Tusipoweka
nguvu ya kutosha katika malezi ya watoto tutakuwa huo ustawi wa watoto
hatuupati, ustawi wa mtoto maana take apate huduma zote za msingi
ikiwemo chakula, malazi, elimu muda wa kukaa karibu na wazazi, walezi
wake , Usimamizi wa haki za mtoto unaanzia kwa mazazi mlezi na jamii
yote kwa ujumla kwa mujibu wa Sheria za nchi yetu jukumu la kuwaangalia
watoto ni la kila raia" alisema Casmiri.
Wakizungumza
mara baada ya kupokea misaada hiyo mkurugenzi wa kituo cha Goodwill
and foundation Sayid Muhzari Aidarus na mlezi wa kituo cha Nyumba ya
Furaha Sister Sarah Francis wameeleza hisia zao juu ya msaada hi
uliotolewa na halmashauri wakiwataka wadau na wahisani mbalimbali
kuendelea kujitokeza kusaidia watoto waliopo katika vituo hivyo hii Ni
kutokana na mahitaji yao huku vituo vikielemewa kutokana na uchumi
mdogo.
"Kwa niaba ya
taasisi niwapongeze na niwashukuru sana kwaajili ya tukio hili adhimu na
lenye thamani juu ya mtoto, watoto Hawa Wana ufahamu na pale wanapoona
jamii haiitikii kuja kwao wanahisi kwamba wametengwa kwahiyo tusipokuja
Kama hivi Tutajenga Taifa la watu wenye roho mbaya na roho ngumu kwa
sababu wataona hawapotezi chochote kwahiyo kuja kqenu mmewakilisha
mamilioni ya watanzania" alisema Aidarus.
"Kwa
niaba ya masister na watoto wa kituo cha Nyumba ya Furaha tunashukuru
sana kwa yale yote ambayo mmetutendea Kama serikali katika kituo chetu
na vituo vyote ambavyo mnatoa misaada hii Hawa watoto tuliokuwepo nao
Wana mahitaji ya vitu vingi na hqki zao za msingi zinatakiwa zitolewe
Kama watoto wengine waliolelewa na wazazi wawili" alisema Sister Sarah.
Siku
ya mtoto wa Afrika ambayo huadhimishwa kila mwaka ifikapo June 16 na
mwaka huu umebebwa na kauli mbiu ya "Zingatia usalama wa mtoto katika
ulimwengu wa kidigital".
Katibu tawala wilaya ya Tanga Mikaya Dalmia kimkabidhi mmoja wa watoto wanaolele katika kituo cha malezi cha Nyumba ya Furaha Net kilichopo jijini Tanga za Mbu zilizotolewa na halmashauri ya jiji la Tanga kwenye madhimisho ya siku ya mtoto wa wa Afrika.
Mlezi wa kituo cha masista cha Nyumba ta Furaha akzungumza mara baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula vilivyotolewa na halmashauri ya jiji la Tanga kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila mwaka june 16.Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Simon Mdende halmashauri ya jiji la Tanga akizungumza mara baada ya kukabidhi vitu mbalimbali ikiwemo chakula kwa vituo sita vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ikiwa ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika.
Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha Goodwill anfa Foundation Sayid Muhzari Aidarus akitoa shukrani mara baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula vilivyotolewa na halmashauri ya jiji la Tanga kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila mwaka june 16.
Mlezi wa kituo cha masista cha Nyumba ta Furaha akzungumza mara baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula vilivyotolewa na halmashauri ya jiji la Tanga kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila mwaka june 16.Mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Simon Mdende halmashauri ya jiji la Tanga akizungumza mara baada ya kukabidhi vitu mbalimbali ikiwemo chakula kwa vituo sita vya kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu ikiwa ni maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika.
Mkurugenzi mtendaji wa kituo cha Goodwill anfa Foundation Sayid Muhzari Aidarus akitoa shukrani mara baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula vilivyotolewa na halmashauri ya jiji la Tanga kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila mwaka june 16.

Mmoja wa watoto wanaolelewa katika kituo cha malezi cha chumba ya Furaha iliyopo jijini Tanga akitoa shukrani mara baada ya kupokea msaada wa vitu mbalimbali ikiwemo chakula vilivyotolewa na halmashauri ya jiji la Tanga kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika inayoadhimishwa kila mwaka june 16.
Post A Comment: