Mhifadhi Robert Faustine katika shamba la miti Meru USA ambalo lipo chini ya TFS, wakiwa wameshiriki kwenye zoezi hilo la upandaji miti kutokana na umuhimu wa pekee haswa katika mifumo ya Ikolojia.
Fransis Nyamhanga ni Afisa Mzingira Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira Kanda Kaskazini (NEMC):Sisi ni wadau wakubwa sana wa mazingira kwahiyo tunapokuwa na wadau kama hawa wanakuja kusapoti masuala ya uhifadhi wa mazingira tunafurahi.
Damian Sulumo ni afisa program wa vikundi vya wakulima na wafugaji( MVIWAARUSHA) Anasema kuwa halmashauri ya Arusha ni wilaya amabayo imeumia na mabadiliko ya tabia nchi hivyo wanalo jukumu la kutunza mazingira
Mkurugenzi mtendaji wa Arusha Dc Suleiman Msumi akipanda mti kama muendelezo wa kampeni hiyo Mwanafunzi wa darasa la saba Jeremia samweli aipanda mti kama muenelezo wa kampeni hiyo inayomtaka kila mtu kufanya hivyo na kuhakikisha kuwa anautunza hadi unakuwa mkubwa
Na.Vero Ignatus,Arusha
Mwendelezo wa Kampeni ya upandaji miti katika halmashauri ya wilaya ya Arusha umezidi kushika kasi ambapo leo tar 11/4/2023 Zaidi ya miti 10,000 ya aina mbalimbali imeoteshwa katika Kijiji cha Losikito na Imbibia,ikiwa kampeni hiyo ni endelevu yenye kauli mbiu isemayo ''Mti wangu Taifa langu mazingira yangu kazi iendelee''
Akizunmza wakati wa upandaji miti katika shule ya Msingi/ sekondari Losikito Mkurugenzi mtendaji wa Arusha Dc Suleiman Msumi alisema kuwa dhamira kuu ni kutokomeza tatizo la ukame,kutunza vyanzo vya maji, pamoja na kutunza mazingira ambapo kila mtu anapaswa kupanda miti na kuwa na zoezi endelevu na kuhakikisha kuwa mti uliopandwa unatunzwa hadi unakuwa mkubwa
‘’Hapa shuleni kila mwanafunzi anapaswa kupanda mti wake na kuhakukisha kuwa anautunza hadi anamaliza elimu ya msingi,sambamba na wanafunzi wa sekondari nao wanatakiwa kufanya hivyohivyo kwasababu tunataka tuwe na miti mingi tutunze mazingira yetu tupate mvua zenye tija na kuepuka majanga yasiyokuwa na sababu yeyote’’Alisema Msumi.
Msumi amesema kuwa wamefanya hayo kwa kutekeleza maagizo ya viongozi wa nchi Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan ,ambaye ni mdau mkubwa wa utunzaji wa mazingira kwani tangia akiwa makamu wa Rais aliweza kuendesha kampeni mbalimbali ikiwemo ile ya kuifanya Dodoma kuwa ya kijani, hivyo na wao wameitikia wito wa kutunza mazingira kwa kupanda miti,pamoja na Waziri mwenye dhamana ya Maziringa na Muungano Dkt.Suleiman Jafo alisisitiza kila Halmashauri shule,taasisi,kuanza ngazi ya familia lazima kupanda miti
Katika kupanda miti kupanda miti kuna masuala mawili lakwanza ni kupanda miti lingine je hiyo miti itaendelea kudumu ,itaendelea kukua? Hivyo kila mmoja anao wajibu wa kuhakikisha miti hiyo tunaihudumia hadi inakuwa mikubwa ikitokea imekufa basi tunabadilisha na kupanda mti mwingine mbadala .Alisema Msumi

Akizungumza kwa niaba ya Kamishana ya Uhifadhi Tanzania Profesa Silayo ,Mhifadhi Robert Faustine katika shamba la miti Meru USA ambalo lipo chini ya TFS, amesema kuwa wameshiriki kwenye zoezi hilo kutokana na umuhimu wa pekee haswa katika mifumo ya Ikolojia ambapo wao wanahudumia shamba la miti Meru ambapo wanatunza mimea bayounuai,vyanzo vya maji pamoja na udongo
Ni wajibu wetu kuhakikisha tunatunza mnyororo mzima wa Ikolojia ili kila mmoja aweze kunufaika na vile vyanzo vya maji mimea pamoja na mazingira safi yanayofanaa kwa afya ya kila mtu,tunashiriki kwa kugawa miti,na kutatoa wito kwa kila mtu mmoja kutunza miti hiyo.
Fransis Nyamhanga ni Afisa Mzingira Baraza la Taifa la Uhifadhi na Usimamizi wa Mazingira Kanda Kaskazini (NEMC):Sisi ni wadau wakubwa sana wa mazingira kwahiyo tunapokuwa na wadau kama hawa wanakuja kusapoti masuala ya uhifadhi wa mazingira tunafurahi na kuwatia moyo ndiyo maana tumefika maeneo haya kushirikiana na wadau hawa wanaochochea sana ikolojia ilikuhakikisha kwamba tunalima lakini wakati huohuo tunahifadhi mazingira
Aidha ametoa Rai kwa wananchi kuhakikisha kuwa miti waliyoipanda wanaitunza ili ije kuwa faida kwao na kwa kizazi kijacho baadae ,kutakuwa hakuna maana yeyote kama tunapanda miti halafu miti hiyo isitunzwe.Alisisitiza Nyamhanga
Damian Sulumo ni afisa program wa vikundi vya wakulima na wafugaji( MVIWAARUSHA) Anasema kuwa halmashauri ya Arusha ni wilaya amabayo imeumia na mabadiliko ya tabia nchi hivyo wanalo jukumu la kutunza mazingira kwa kupanda miti hadi itakapofikia mwisho wa mradi wao KILIMO ENDELEVU wawe wameweza kufikia hekta 60 sawa na heka 160,hivyo wataendelea kuhamasisha wakulima na wafugaji waweze kupanda miti maeneo ya wazi na mashambani na kutunza mazingira
Aidha amesema kuwa mradi huo unawezesha shughuli hizo sambamba na wadau wengine waliopo kuweza kuhakikisha wanafanya shughuli nyingine za uzalishaji ambapo shughuli hiyo ni ya mwendelezo
Ayesiga Buberwa ni meneja miradi wa shirika la ISLAND OF PEACE,pamoja namashirika mengine mawili wanatekeleza mradi wa kilimo endelevu Arusha unaolenga kukuza na kuendeleza kulimo ekolojia kwa watu pia linaangalia chakula kinapoanza shambani hadi kinapofika kwa mlaji mazingira yanayomzunguka sambamba na utunzaji na uhifadhi wa mazingira
Buberwa amesema kuwa wanaangalia mifumo yote ya uzalishaji wa chakula pamoja na ile ya kuhifadhi mazingira kwamba mradi huo unaangalia kuuhisha katika hali ya kawaida mazingira ambayo yameharibika il mkulima aweze kulima vizuri pamoja na mfugaji aweze kufuga vyema pia na malaji aweze kupata chalila safi na salama.
Post A Comment: