Mbunge wa Jimbo la Kilolo mkoani Iringa Justine Nyamoga akiongea wakati wa zoezi la uchangishaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi ya Huruma Center.
Askofu wa KKKT Dayosisi ya Iringa Blastoni Gavile akiongea wakati wa zoezi la uchangishaji wa fedha kwa ajili ya ujenzi wa shule ya msingi ya Huruma Center
Mbunge wa Jimbo la Kilolo mkoani Iringa Justine Nyamoga akiwa sambamba na Askofu wa KKKT Dayosisi ya Iringa Blastoni Gavile wakiwa viongozi mbalimbali katika eneo la ujenzi wa shule ya msingi ya Huruma Center.


Na Fredy Mgunda, Iringa

MBUNGE wa Jimbo la Kilolo, Mkoani Iringa Justine Nyamoga ameongoza harambee kwa ajili ya kuchangia ujenzi wa Shule ya Msingi matika Kituo cha Watoto Yatima cha Huruma.


Kituo hicho kinachomilikia na Kanisa la Kiinjili la Kirutheli Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Iringa mbali na watoto yatima kimekuwa kikihudumia watoto waliofanyiwa ukatili ikiwemo ulawiti na ubakaji.


Akizungumza katika harambee hiyo aliyokusanya zaidi ya Sh40 Milioni, Nyamoga ameishauri jamii kujitoa kwa ajili ya kuwasaidia watoto walio katika mazingira magumu.


Kwa upande wake Askofu wa KKKT Dayosisi ya Iringa Blastoni Gavile alimpongeza Nyamoga kwa upendo na kukubali wito wa kushiriki harambee hiyo.


"Hiki ni kituo chetu wenyewe tunapaswa sisi tuanze kujitoa kuliko wengine, Kuna Baraka nyingi unachuma unapotoa," amesema Nyamoga.


Askofu Gavile alisema lengo laa kituo hicho ni kuwapa uhakika wa elimu watoto wanao walenda ndani ya kituo.


"Mungu akubariki sana Mbunge wetu kwa utayari wako kuja kuwasaidia watoto Hawa," amesema Askofu Gavile.

Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: