Dkt Tumaini Msowoya akizungumza na wanafunzi wa kidato cha sita na pembeni ni Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mbalamaziwa, Sister Revina Kilai
Dkt Tumaini Msowoya akizungumza na wanafunzi wa kidato cha sita na pembeni ni Makamu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Mbalamaziwa, Sister Revina Kilai
Dkt Tumaini Msowoya akifurahia jambo na wanafunzi wa kidato cha sita Shule ya Sekondari ya Mbalamaziwa.

Na Fredy Mgunda, Iringa.


Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Iringa Dkt Tumaini Msowoya amewaasa wasichana wa kidato cha sita  kuwekeza katika bidii, utii na kumcha Mungu kama ngao yao ya mafanikio.


Dkt Msowoya alikuwa mgeni rasmi kwenye mahafari ya kidini ya TYSS,  kwa wanafunzi wa kike wa kidato cha sita katika  Shule ya Sekondari ya Mbalamaziwa, Wilayani Mufindi, Mkoani Iringa.


"Hata ukifaulu kwa alama za juu sana kama sio mtii, humchi Mungu bidii yako ni bure tu," amesema.


Mjumbe huyo wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Iringa pia aliwapongeza walimu na viongozi wa Kanisa la Roman Katholiki kwa kuwafundisha wanafunzi hao katika msingi wa maadili kiasi cha kuwafanya wajitambue.


Awali, Paroko wa Patokia ya Nyakipamba, Padre Kizito Fungo aliwaasa wahitimu hao kumtanguliza Mungu katika kila jambo.


Nae Makam Mkuu wa Shule ya Sekondari ya  Mbaramaziwa, Sister Revina Kilai amesema wanafunzi hao wameandaliwa vizuri tayari kwa kukabiliana na mitihani.

Share To:

mwangaza wa hbari

Post A Comment: