Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,Prof.Mohamed Janab akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 13,2022 Jijini Dar es Salaam. Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Damu na Mkuu wa Kitengo cha Wagonjwa wa Damu Muhimbili Dkt.Stella Rwezaula akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 13,2022 Jijini Dar es Salaam.Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto Dkt.Victor Mgotta akizungumza na waandishi wa habari leo Desemba 13,2022 Jijini Dar es Salaam.

******************

NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Kwa mara ya Kwanza,Kambi rasmi maalum ya Tohara Salama kwa wanaume imeanza Disemba 12 mwaka huu hadi Disemba 16, inayotolewa na Hospital ya Taifa Muhimili kwa kushirikiana na wataalamu kutoka nchini Kenya.

Akizungumza na Waandishi wa Habari leo Desemba 13,2022 Jijini Dar es Salaam, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili,Prof.Mohamed Janab amesema kuwa kambi hiyo itawahusisha wagonjwa 25 wenye changamoto ya uvujaji wa damu na kwenda sambamba na utoaji wa mafunzo kwa wataalamu nane kutoka Hospitali mbalimbali za Tanzania zenye kliniki ya Himofilia.

"Aina ya upasuaji utafanyika kwa njia tofauti na ilivyozoeleka kwani wagonjwa hawa wanahitaji uangalizi wa karibu ili kuepuka athari ya kupoteza damu,pia mgonjwa atahitajika kulazwa kwa muda wa siku tano hadi saba". Amesema Prof.Janab.

Amesema tangu kuanzishwa kwa miradi wa kuongeza kasi ya upatikanaji huduma kwa wagonjwa wa damu, umefanikiwa kwa kuzindua kliniki ya Himofilia nchini katika hospitali mbalimbali, mafunzo kwa watoa huduma za afya wapatao 548, mafunzo ya nje ya nchi kwa wataalamu saba pamoja na manunuzi ya vifaa vya maabara.

Amemaliza kwa kusema kubwa Hospitali ya Taifa Muhimbili itaendeleza kampeni za aina hiyo ili kuendelea kuboresha huduma na kuzidi kuwajengea uwezo wataalamu.

Kwa upande wake Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Damu na Mkuu wa Kitengo cha Wagonjwa wa Damu Muhimbili Dkt.Stella Rwezaula amesema kuwa kuwa zaidi ya watanzania 5800 wana tatizo la haemophinia bila kujua kuwa wanatatizo hilo.

Aidha Dkt.Stella amewashauri watu kuacha imani za kishirikina, wasiende kwa waganga wa kienyeji pale wanapomuona mgonjwa anayetokwa damu puani, au anayetokwa na damu isivyokawaida aking'olewa jino au baada ya kufanyiwa tohara n.k, bali waende kwa wataalamu wa afya ili wapewe matibabu sahihi.

Naye Daktari Bingwa wa Upasuaji wa Watoto Dkt.Victor Mgotta ametoa wito kwa wanaotokwa na damu bila udhibiti wajitokeze kwenye vituo vya afya vya kanda ili waweze kupatiwa matibabu.

Hoemophibia ni ugonjwa wa kutokwa damu bila ukomo, ambapo imeelezwa kuwa asilimia 70 ya wagonjwa hurithi kutoka kizazi hadi kizazi, na asilimia 30 hupata kutokana na mabadiliko ya vinasaba.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: