Afisa Udhibiti Ubora (TBS) Bi. Hidaya Kabelege akitoa elimu kuhusu madhara ya vipodozi vyenye viambata sumu na usajili wa bidhaa na majengo ya chakula na vipodozi kwa wananchi waliotembelea banda la TBS lililopo katika tamasha la siku ya vipodozi 2022, lililofanyika katika viwanja vya Leaders Club, Kinondoni, Dar es Salaam mapema leo.

*****************

SHIRIKA la Viwango Tanzania (TBS) limeshiriki katika Tamasha la Siku ya Vipodozi 2022 katika Viwanja vya Leaders Club Jijini Dar es Salaam ambapo wananchi wameweza kutembelea kwenye banda la TBS na kupewa huduma.

TBS imetoa elimu kuhusu madhara ya vipodozi vyenye viambata sumu na usajili wa bidhaa na majengo ya chakula na vipodozi kwa wananchi ambao wameweza kutembelea kwenye Tamasha hilo.

Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: