Kituo cha Umahiri cha Kilimo Sayansi ya Chakula na Usalama wa Lishe ( CREATES – FNS) kilichopo katika Taasisi ya Afrika Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela kimekuwa mstari wa mbele katika kutimiza mpango wa Ushirikiano baina ya Serikali na Sekta binafsi (PPP) kwa kuzalisha bidhaa ambazo zimesaidia kutatua changamoto za jamii.
Akizungumza na wananchi waliotembelea banda la Taasisi ya Nelson Mandela katika maonyesho ya 28 ya nanenane Themi Jijini Arusha, Meneja wa CREATES-FNS Bi. Rose Mosha ameeleza kuwa mojawapo ya bidhaa iliyozalishwa na kituo kwa kushirikisha sekta binafsi ni Dawa ya NUSA iliyotengenezwa na miti dawa ya asili ambayo ni kinga dhidi ya homa kali ya mfumo wa upumuaji, ugonjwa wa pumu, kuondoa nyama za puani na kuongeza kinga mwilini katika kupambana na magonjwa ambayo imesajiliwa na Baraza la Tiba Asili Tanzania.
Bi. Rose anazidi kueleza kuwa bidhaa nyingine ni Buheri wa Afya ambayo ni dawa iliyotengenezwa na miti dawa asili inayoondoa homa kali ya mfumo wa upumuaji unaosababishwa na virusi na kuongeza mfumo wa kinga mwilini pamoja na kurekebisha magoinjwa ya moyo na kisukari.
“Dawa hizi zimezalishwa kwa ushirikiano wa Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela kwa kushirikiana na Tanzania Healthy Laboratory Service Solutions Organization kupitia mpango shirikishi baina ya serikali na sekta binafsi” amesema Bi. Rose Mosha
Naye Simprosa Ngawa mmoja wa wananchi waliotembelea banda hilo ametoa pongezi kwa kituo cha CREATES-FNS pamoja na Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela kwa kuwa mstari wa mbele kutoa bunifu ambazo zinatatua changamoto zinazoikabili jamii.
Post A Comment: