Mkuu wa Wilaya ya Simanjiro Dkt. Suleiman Serera ameipongeza Taasisi ya Afrika ya Sayansi na Teknolojia ya Nelson Mandela kwa kuleta mapinduzi katika sekta ya elimu ya juu hususani eneo la utafiti na Ubunifu.
Dkt. Serera ametoa Pongezi hizo, Agosti 7, 2022 alipotembelea banda la Taasisi hiyo katika maonesho ya nane nane kanda ya Kaskazini viwanja vya Themi Arusha .
"Wito wangu kwa taasisi ni kuendelea kuatamia wabunifu tangu wakiwa wadogo ili kuwaendeleza na kupata watafiti wazuri na wabobezi katika kutatua changamoto zinazoikabili"amesema Dkt. Serera
Alizidi kueleza kuwa, Serikali itazidi kushirikiana na taasisi hiyo katika kuhakikisha vipaji vya watafiti na wabunifu vinaendelezwa, na kuzidi kuleta chachu ya maendeleo kwa jamii.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya Maandalizi ya Nane Nane kutoka Taasisi hiyo, Prof. Gabriel Shirima ameahidi kufanyia kazi ushauri katika kuboresha eneo hilo la Utafiti na Ubunifu.
Dkt. Serera alipata fursa ya kuongea na wananchi waliohudhuria mafunzo ya Kilimo Endelevu kukabiliana na Mabadiliko ya Tabia ya nchi, yanayotolewa bure na taasisi hiyo, na kuwataka wananchi hao kutumia fursa hiyo adimu ili kuboresha kilimo.
Post A Comment: