Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Theobald Sabi (Kulia) akisalimiana na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja Ofisa Mkuu wa Uendeshaji Benki ya NBC Bi Alelio Lowassa (wa pili kushoto) na Mkuu wa Kitengo cha Uhusiano wa NBC, Godwin Semunyu


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa akizungumza na wageni waalikwa wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki ya NBC jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Theobald Sabi akizungumza na wageni waalikwa wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki ya NBC jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Theobald Sabi (Kushoto) akisalimiana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Dkt. Hassan Abbasi wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Theobald Sabi (Kulia) akisalimiana na wageni mbalimbali akiwemo Balozi wa Uingereza nchini Mhe. David Concar (katikati) wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Theobald Sabi (Kulia) akisalimiana na Mbunge wa Jimbo la Muheza Mkoani Tanga Mhe, Hamisi Mwinjuma (Mwana FA) wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Ofisa Mkuu wa Uendeshaji Benki ya NBC Bi Alelio Lowassa (kulia) akisalimiana na baadhi ya wageni wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki hiyo jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.


Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa (Katikati) akiwa kwenye picha ya pamoja na wadau mbalimbali wa sekta ya michezo, sanaa na utamaduni nchini wakati hafla ya jioni iliyolenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza iliyoandaliwa kwa ushirikiano na benki ya NBC jijini Dar es Salaam mwishoni mwa wiki.

..............................................

Benki ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza kuhusu adhma yake ya kukuza na kuendeleza sekta ya michezo hapa nchini kwa kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanywa na serikali pamoja na wadau wengine wa sekta hiyo inayokua kwa kasi.

Akizungumza kwenye hafla ya jioni iliyofanyika mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam ikilenga kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola yaliyofanyika hivi karibuni Birmingham, Uingereza, Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya NBC Bw. Theobald Sabi alisema sekta ya michezo, sanaa na utamaduni ina mchango muhimu katika suala zima la ajira pamoja na kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na pato la taifa kwa ujumla.

“Pamoja na kuitikia wito wa serikali katika kuinua sekta hii muhimu, benki ya NBC tumebaini kwamba sekta hii ni eneo la kimkakati kiuchumi iwapo sisi kama wadau muhimu tutaiunga mkono,’’ alisema Bw Sabi kwenye hafla hiyo iliyohudhuliwa na wadau mbalimbali wa sekta hiyo wakiwemo viongozi waandamizi wa serikali wakiongozwa na Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mhe. Mohamed Mchengerwa.

Bw Sabi alibainisha kuwa benki hiyo Ina dhamira ya dhati ya kushirikiana na wadau wa sekta michezo, sanaa na utamaduni na dhamira hiyo inapimwa kwa namna ambavyo taasisi hiyo hiyo inadhamini matukio mbalimbali ya kimichezo hapa nchini ikiwemo Ligi Kuu ya Tanzania Bara (NBC Premier League), NBC Dodoma Marathon, mashindano mbalimbali ya mchezo wa golf pamoja na kuunga mkono jitihada za ujenzi wa miundombinu ya michezo ikiwemo ujenzi wa viwanja vya mpira katika maeneo mbalimbali nchini.

“Hivyo basi kwetu NBC milango ipo wazi wa wadau mbalimbali wa sekta ya michezo, sanaa na burudani ili tuweze kushirikiana katika kukuza sekta hii muhimu lengo likiwa ni kukuza ajira ambayo ni nyenzo muhimu kiuchumi na ustawi wa sekta ya fedha nchini,’’ alisema.

Pamoja na kuwapongeza na kuwakaribisha wanamichezo wa Kitanzania walioshiriki kwenye Mashindano ya Jumuiya ya Madola hafla hiyo pia ilihusisha makabidhiano ya taarifa ya namna bora ya kusimamia HAKIMILIKI na ugawaji wa Mirabaha kwa wamiliki wa kazi za sanaa nchini.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: