Naibu Waziri wa Nifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akiweka Saini kwenye kitabu cha kumbukumbu mara baada ya kutembelea Banda la maonesho la Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) Mapema Jana Jijini Dar es salaam 

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akipata Maelezo katika Banda la COSTECH kwenye viwanja vya maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es salaam Mapema Jana picha zote na Afisa Habàri na Mahusiano COSTECH Faisal Abdul Jalil. 


Na Ahmed Mahmoud. 


NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Mhe. Abdalah Ulega amesema kuwa kuna haja ya Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kuongezewa nguvu ili waweze kuisaidia Nchi ya Tanzania kwa kuwashika mkono watafiti na wabunifu mbalimbali ambao wanabuni bunifu zenye tija kwa Taifa.


Naibu Waziri Ulega amesema hayo leo Jumanne Julai 5, 2022 alipotembelea Banda la COSTECH katika Maonesho ya 46 Kimataifa ya Biashara Dar es salaam maarufu kama Sabasaba - Jijini Dar es Salaam.


Akiwa katika banda hilo Ulega amewashauri Watanzania kutembelea Banda la COSTECH kwaajili ya kushuhudia bunifu mbalimbali zilizobuniwa na Watanzania wenzetu.


" Nimeona kazi nzuri sana zinazofanywa humu ndani nawashauri Watanzania kutembelea banda hili kujionea tafiti mbalimbali za Tanzania" amesema Mhe. Ulega.


Amefafanua kuwa watanzania kutembelea Banda la Tume hiyo katika Maonesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama  Sabasaba ili kuendana na kauli mbiu ya mwaka huu "Tanzania ni mahala sahihi kwa Biashara na Uwekezaji ", viwanja vya Mwl  Nyerere hapa Jijini Dar es Salaam kwaajili ya kujifunza teknolojia mbalimbali kwa manufaa ya nchi yetu.


Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akipata Maelezo Wakati alipotembelea Banda la COSTECH katika viwanja vya maonesho ya Sabasaba

Josephine Sepeku kutoka Atamizi ya DTBI akimpa Maelezo Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega alipotembelea Banda la COSTECH katika viwanja vya maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es Salaam. 


Share To:

Arusha Newsroom

Post A Comment: