MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akizungumza na Bodi ya Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Julius Kalolo wa Pili kulia na Watendaji wa Wakala huo waliofika ofisini kwake kabla ya kuanzia ziara ya kuelekea Kijiji cha Msomera Kata ya Misima wilayani Handeni kushoto ni Katibu Tawala wa Mkoa wa Tanga Pili Manyema

 

Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Julius Kalolo akieleza mpango wa wakala huo katika Kijiji cha Msomera Kata ya Misima wilayanai Handeni mara baada ya kumaliza ziara ya kukitembelea kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Handeni Mashaka Mgeta na kulia ni Mbunge wa Jimbo la  Handeni Vijijini John Salu
Mkurugenzi wa REA Mhandisi Hassan Saidi akizungumza jambo wakati wa ziara hiyo kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Handeni Mashaka Mgeta
Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini (CCM) John Salu akizungumza wakati wa ziara hiyo
KATIBU Tawala wa wilaya ya Handeni Mashaka Mgeta akizungumza wakati wa ziara hiy o kulia ni Mbunge wa Jimbo la Handeni Vijijini John Salu


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Julius Kalolo akitoka kwenye moja ya makazi wa wananchi wa Msomera waliotoka Ngorongoro wakati wa ziara yake  wa kwanza kushoto ni Katibu Tawala wa wilaya ya Handeni Mashaka Mgeta





NA OSCAR ASSENGA,HANDENI

MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima amempongeza Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Julius Kalolo na Watendaji wa Wakala huo kwa kazi nzuri wanayoifanya kwa sababu imekuwa ni sekta inayotolewa mfano kwa Afria nzima kutokana na utendaji wao.

RC Malima aliyasema hayo wakati Mwenyekiti huyo wa Bodi ,Mkurugenzi wa REA na watendaji wengine walipofika kuzungumza na Mkuu wa Mkoa wa Tanga kabla ya kuanza ziara ya kutembelea Kijiji cha Msomera kilichopo wilayani Handeni ili kujionea maendeleo na hali halisi na ili kupata taarifa zitakazoiwezesha bodi kukaa na kuiridhisha mambo muhimu na ya msingi ambayo yatafanya mazingira ya makazi kuwa na mazuri.

Alisema kwamba kutokana na kazi nzuri inayofanywa na wakala huo na kuwa mfano kwa Afrika Nzima zipo taasisi zinatamani kuja kujifunza kazi nzuri mlivyofanya hivyo nitumie fursa hii kuwapongeza sana huku akiwataka kuendeleza kasi hiyo.

“Lakini nichukue ahadi kwamba hao wakandarasi mnaofanya kazi na gharama za vifaa vinavyotumika sio ndogo huu ni uwekezaji mkubwa ambao unafanywa na serikali faida ni wananchi kupata umeme,niwapongeza isipokuwa miradi hiyo ina kipindi cha miwezi 18 wamepewa niwaambie kwamba Serikali ya Mkoa itaendelea kushirikiana nayi kusimamia miradi hii”Alisema

“Katika kikao chetu cha leo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Mtendaji Mkuu wa Rea na wakandarasi wa miradi mbalimbali inayotekelezwa na REA mkoa huo tumepata muda wa kukaa na kushauriana nasuala mbalimbali ya utekelezaji bora wa miradi ya hii kwenye mkoa huo “Alisema

Aidha alisema wapo wanahabari hivyo niwaambie kwenye kazi mbalimbali zinazoendelea hakuna wilaya ilitakayokosa mradi wa rea hilo ndio kubwa na wanamshukuru Rais Samia Suluhu,Wizara ya Nishati na REA kwa kazi kubwa wanayofanya kuhakikisha nchi nzima huduma ya umeme inafika kwa wananchi.

Awali akizungumza wakati akiwa eneo la Msomera wilayani Handeni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Wakili Julius Julius Kalolo alisema kwamba Serikali wa kuomba baadhi ya watu wa Ngorongoro kuhamia eneo hilo kwa vyoyote mahitaji ya nishati vijijini yamekuwa makubwa kuliko ambavyo walivyokuwa wametengeneza kwenye bajeti yao.

Alisema hivi sasa wataweze kupitisha bajeti ya nyongeza kuhakikisha miundombinu ya nishati katika eneo la Msomera inakwenda vziuri kwa kuzingatia mfumuko wa wakazi wa eneo hilo ilikuwa lazima yeye na Mkurugenzi wa REA na watendaji wafika waone hali halisi na kupata taarifa kamili ili kuiwezesha bodi kwenye kukaa na kuiridhisha mambo muhimu na ya Msingi.

“Tutafanya mazingira ya makazi kuwa na mazuri na hawatawapa shida kwani wakazi walioamua wenyewe kuhamia eneo hili ili wasione kama wametengwa kilio cha muda mrefu maeneo yake mengi hayana huduma ya nishati vijijiji kwa kuwa hili lilijitokeza wakaona huu ndio wakati wake waende wajione ili waweze kutimiza azma ya kueneza nishati vijijini.

“RC ametupa maagizo ambayo tutakuwenda kuyafanyia kazi kuhakikisha nishati ya umeme inafika Kijiji cha Msomera na maeneo mengine hapa na hii ni hatua ya kwanza lakini bado kuna hatua nyengine ikiwemo mpango mwengine wa kuleta nishati mbadala kwa ajili ya kupikia ili kurahisisha maisha ya waakzi wa eneo hilo”Alisema

Naye kwa upande Mkurugenzi wa REA Mhandisi Hassan Saidi alisema wamefika eneo la Msomera ambacho kimetengwa kwa watanzania kutoka Ngorongoro Arusha na Taasisi mbalimbali zipo hapo kwa ajili ya kutoa huduma na wao wameona wahusike kuboresha huduma ya umeme kutoka kila kilomita 30 na tayari kilomita 15 zimeshakamilika na tano za hapa zimekamilika na Transoma ipo tayari kuwashwa na mradi utaendelea katika maeneo hayo ya msomera.

Mhandisi Hassan alisema mradi ambao wameufanyia kazi ni wa awamu ya tatu mzunguko wa pili kama alivyosema Mwenyekiti huo mradi upo kila kijiji kilipewa kilomita 1 ukiangalia hiyo haitoshi lakini azma yao ni kufikisha huduma ya umeme kwenye vijiji.

Alisema mpango wake ni kuhakikisha vijiji vyote vya Tanzania Bara vinafikishiwa umeme azma ya kwanza ni kufikisha umeme kwenye vituo vikubwa na kusambaza umeme kwenye majumbani wanafanyia kaz.

Hata hivyo alisema serikali imehaidi kuwapatia fedha hivyo wananchi wasiwe na hofu kila kijiji kitapata umeme na wanatarajia kufikia wateja wengi zaidi na kwa mkoa wa Tanga zaidi ya mradi wa Rea 111 ,11 wana mradi wa ujazilizi.

Mwisho.



Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: