Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk.Angeline Mabula akimpatia hatimliki ya kimila Bibi Agnes Mangashini kutoka Jamii ya Wawindaji ya Wahadzabe wa Kijiji cha Munguli Kata ya Mwangeza wilayani Mkalama wakati wa hafla ya kukabidhi hati hizo iliyofanyika jana.Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo,

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk.Angeline Mabula akizungumza katika hafla hiyo.

Mkuu wa Wilaya ya Mkalama ,Sophia Kizigo akizungumza wakati wa zoezi la utoaji hatimiliki hizo.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk.Angeline Mabula na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Sophia Kizigo (kushoto)  wakiserebuka na Wanawake wa Kikundi cha Sanaa cha Jamii ya Wawindaji ya Wahadzabe wa Kijiji cha Munguli Kata ya Mwangeza wilayani Mkalama.
Watoto wakiwa kwenye hafla hiyo.
Diwani wa Kata ya Mwangeza Bosco Samwel akizungumza kwenye hafla hiyo.
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Mkalama, Lameck Itungi akizungumza kwenye hafla hiyo.
Wanawake wa Jamii ya Wahadzabe wakimpa heshima ya kumvika shanga za kimila Dk. Angeline Mabula katika hafla hiyo.
Wanawake wa Jamii ya Wahadzabe wakiwa kwenye hafla hiyo.
Wananchi wa Jamii ya Wahadzabe wakisubiri kupatiwa hati zao.
Hati zikikabidhiwa.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula (katikati) na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo (kulia kwake) na viongozi wengine wakiwa katika picha ya pamoja na wananchi wa Jamii ya Wawindaji ya Wahdazabe  baada ya kuwakabidhi Hatimiliki za  kimila za kumiliki ardhi ambapo hati 100 walikabidhiwa.
Chifu wa Jamii ya Wawindaji ya Wahadzabe Edward Mkumbo akifurahi na Kamishna wa Ardhi Msaidizi  Mkoa wa Singida Shamim Hoza baada ya kukabidhiwa hatimiliki yake.
Wasanii wa kikundi cha Utamaduni cha Jamii ya Wahadzabe wakiwa wamejipanga kwa ajili ya kutoa zawadi kwa Dk. Mabula na viongozi wengine meza kuu.
Dk. Mabula akipokea zawadi ya asali.
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula akizungumza baada ya kupata maelezo ya ujenzi wa jengo la makumbusho la Jamii ya Wawindaji ya Wahadzabe kutoka kwa Diwani wa Kata ya Mwangeza, Bosco Samweli (kulia) ambapo aliahidi kuchangia mifuko hamsini ya saruji. 
 Katibu Tawala wa Wilaya ya Mkalamam Elizabeth Rwegasi akitoka kwenye nyumba ya Chifu wa jamii hiyo wakati wa ziara ya utoaji hatimiliki za kimila

Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dk. Angeline Mabula akitoka kwenye nyumba ya Chifu wa jamii hiyo wakati wa ziara ya utoaji hatimiliki za kimila. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Mkalama, Sophia Kizigo.

Sara Abel kutoka Jamii ya Wahadzabe akimpatia maji mtoto wake Kizali George wakati wa hafla hiyo.Sara ni mmoja wa jamii hiyo waliopata hatimiliki ya ardhi ambayo ndio urithi wa baadaye wa mtoto huyo baada ya masomo.
 

 

Na Dotto Mwaibale, Singida


JAMII  ya Wawindaji ya Wahadzabe iliyopo Wilaya ya Mkalama mkoani Singida imeipongeza Serikali kwa hatua iliyoichukua ya kuwapimia maeneo yao na kupatiwa hatimiliki za kimila na kuwa sasa wataacha maisha ya kuhamahama na kujikita katika shughuli za maendeleo.

Kupata kwa hatimiliki hizo kunafungua milango ya fursa kwa jamii hiyo inayojishughulisha na uwindaji huku chakula chao kikiwa ni matunda pori, asali na uchimbaji wa mizizi ambayo waitumia kama chakula na dawa kwa ajili ya kujitibu.

Hatua hiyo ya kuwapimia ardhi na kuwapatia hatimiliki inamfanya kila Muhadzabe kumiliki ardhi yake hivyo kuepusha kabisa na uwezekano wa kugombea maeneo ya uwindaji na shughuli zingine zinazohitaji matumizi ya ardhi.

Akizungumza jana katika hafla ya kukabidhiwa hati 100  na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Dkt Angeline Mabula  kwa niaba ya wenzake Mwenyekiti wa jamii hiyo, Edward Mkumbo alisema sasa wameacha kabisa kuhamahama kama ilivyokuwa awali na kuwa  wameanza kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo tofauti na zamani.

"Tunaishukuru Serikali ya  Rais wetu Samia Suluhu Hassan kwa kutuletea jambo ili zuri na kuitambua jamii yetu na kutupimia ardhi yetu itatusaidia kwani tayari tulisha anza kuvamiwa na wafugaji kutoka mikoa mingine na kutushia mustakbari mzima wa maisha yetu" alisema Mkumbo.

Akizungumza na jamii hiyo ya wawindaji ya Wahadzabe katika Kijiji cha Munguli, Kitongoji cha Kipamba Kata ya Mwangeza wilaya humo Dk.Mabula alisema, jamii hiyo ni miongoni mwa jamii ndogo nchini ambayo iko katika hali ya kupoteza ardhi wanayoimiliki kutokana na jamii nyingine kuingia na kufanya shughuli zisizoendana na tamaduni za jamii hiyo jambo alilolieleza linahatarisha ustawi na maisha na desturi za Wahadzabe na kuwa Serikali haitakuwa tayari kuona jambo hilo likitokea.

 ‘’Serikali haitakubali kuona ardhi inayotumiwa na jamii hiyo ikipotea kwani katika miaka ya hivi karibuni jamii ya Wahdzabe  imekuwa ikikabiliwa na tishio la kutoweka na kupoteza uhalisia wa maisha yao baada ya baadhi ya wananchi kutoka maeneo mengine kuingia katika maeneo ya mapori ya asili wanayoyatumia na kuanza kuyavamia kwa ajili ya shughuli za ufugaji, kilimo na  upasuaji wa mbaoi’’ alisema Dk. Mabula

Alitaja baadhi ya matishio ya maeneo hayo ni kuanza kupotea  kwa makazi ya asili yanayojengwa kwa nyasi kavu chini ya matawi ya miti, wanyama kutoweka, mizizi na matunda kupotea kutokana na mabadiliko ya tabia nchi na shughuli nyingine ambazo hazilindi uoto wa asiili wa mapori hayo.

Dk.Mabula alisema  kwa kutambua athari inayoweza kujitokeza dhidi ya jamii hiyo Serikali kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wanatafuta  njia bora ya kulinda jamii hiyo na wananchi wengine ili kuhakikisha kuna kuwa na usawa kwa wote katika matumizi ya rasilimali za ardhi hapa nchini.

Aidha Dk.Mabula alitumia nafasi hiyo kumpongeza Mkuu wa Mkoa wa Singida Dk.Binilith Mahenge na watendaji wote wa idara ya ardhi mkoani hapa na wilaya ya Mkalama hasa Kamishna wa Ardhi Msaidizi i Mkoa wa Singida Shamim Hoza kwa kufanikisha mpango huo.

Mkuu wa wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo alisema, jamii ya Wahadzabe katika eneo hilo la Kijiji cha Munguli Kata ya Mwangeza na baadhi ya maeneo kumekuwa  na changamoto ya migogoro ya ardhi hasa  inayohusu mipaka.

‘’Changamoto yetu kubwa hapa, jamii ya Wahadzabe vyakula wanatoa porini, wanakula asali na nyama za kuwinda na misitu ikiharibiwa au maeneo wanayotegemea kupata vyakula yanapoharibiwa ni changamoto kubwa, hata hivyo nichukue nafasi hii kuwapongeza kwa uvumilivu wao wa muda mrefu’’ alisema Kizigo.

Katika hafla hiyo baadhi ya wananchi wa eneo hilo walipata fursa ya kuzungumzia changamoto mbalimbali za migogoro ya ardhi akiwemo Diwani wa Kata ya Mwengeza Bosco Samweli, ambaye alimueleza  Dk Mabula kuwa, eneo hilo la jamii ya Wahadzabe kwa muda mrefu limekuwa na changamoto ya migogoro ya mpaka na wananchi wanaoishi wilaya za jirani za Karatu Arusha na Mbulu mkoa wa Manyara na kuwa sasa zinaelekea kumalizika kutokana na juhudi kubwa inayofanywa na Mkuu wa Wilaya ya Mkalama Sophia Kizigo ya kuzitatua akishirikiana na maafisa ardhi wa wilaya hiyo na wataalam wengine. 

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: