Na Mwandishi wetu Loliondo.


MKUU wa Jeshi la Polisi nchini IGP Simon Sirro leo  amefanya ziara katika eneo la Loliondo, Ngorongoro kwa ajili ya kujionea zoezi linaloendelea la uwekaji alama za mipaka, ambapo ameeleza kuridhishwa kwake na kasi iliyopo.

IGP Sirro ambaye alifuatana na Mkuu wa Mkoa wa Arusha John Mongella, amewataka washiriki wa zoezi hilo kujituma ili kazi ya uwekaji alama za mipaka katika eneo hilo iishe kwa wakati.

Sirro amesisitiza wananchi kuwa watulivu na kushirikiana na serikali katika uamuzi huu wenye lengo la kuhifadhi eneo hilo kwa faida mtambuka za nchi.

'Msikubali kutumika kuchochea vurugu ambazo hazina manufaa kwa pande zote  na wala msikubali kutumika kwa niaba ya wale wote wasiotutakia mema kama taifa', alisema Sirro.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. John Mongella alimhakikishia IGP Sirro kuwa Serikali ya Mkoa wa Arusha imejipanga kuhakikisha kuwa zoezi linaendeshwa kwa hali ya utulivu kwa kuzingatia sheria za nchi.




Share To:

Post A Comment: