MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akizungumza mara baada ya mazungumzo hayo
MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akizungumza na ujumbe huo
              
MKUU wa Mkoa wa Tanga Adam Malima akizungumza na ujumbe huo
 Serikali imetenga Sh bilioni 15 kwa ajili ya ujenzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe mkoani Tanga.
Makamu
 Mkuu wa chuo hicho, Profesa Lughano Kusihika amesema hayo wakati yeye 
na ujumbe wake ulipokutana na Mkuu wa Mkoa wa Tanga kwa ajili ya 
mazungumzo na kujadiliana eneo la kujenga chuo hicho.
Alisema
 serikali kupitia Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imeamua kwamba 
Chuo Kikuu cha Mzumbe kishiriki katika kuanzishwa kwa chuo kikuu katika 
Mkoa wa Tanga na kwamba fedha kwa ajili ya shughuli hiyo ni mkopo wa 
masharti nafuu kutoka Benki ya Dunia (IMF) kwa ajili ya kuboresha 
miundombinu na rasilimali watu na Mzumbe ni moja kati ya vyuo ambavyo 
vimepata fursa hiyo.
“Kwa 
ajili ya kuanzisha kampasi ya Tanga zimetolewa Sh bilioni 15 kwa hiyo 
tuko katika maandalizi ya kufanya shughuli hiyo na sisi kama Mzumbe 
tumefurahi kwa heshima ambayo tumepewa Mkoa wa Tanga ya kuja kuanzisha 
kampasi yetu hapa.
“Mkoa wa 
Tanga wote tunaufahamu ni mkoa mkubwa ambao una mambo mengi na huko 
nyuma ulikuwa ni maarufu sana kwa ajili ya viwanda na wote tunajua 
kwamba serikali yetu inataka kujenga uchumi wa viwanda, kwa hiyo sisi 
ambao tuko katika vyuo vikuu tunatakiwa tushiriki kikamilifu katika 
shughuli hii na mradi wenyewe kwa ujumla wake unafadhiliwa na IMF kwa 
mageuzi ya kiuchumi,” alisema.
Alitaja
 lengo kubwa la serikali ni kuangalia namna gani vyuo vikuu 
vitashirikiana na jamii katika maeneo mbalimbali kuendesha programu na 
kujenga uwezo kwenye maeneo hayo na kufanya shughuli ambazo zitaleta 
mageuzi.
Profesa Kusihika 
alisema bado wanaendelea na majadiliano ya kupata eneo ambalo wanaweza 
kuanza ujenzi ambapo alifafanua zaidi lengo la serikali ni kuanzisha 
kampasi na kuikuza halafu huenda huko mbeleni ikafika mahala ikawa ni 
chuo kikuu kinachojitegemea.
“Kwa
 hiyo tunawaomba sana wakazi wa Mkoa wa Tanga na viongozi wao, wapokee 
hili wazo zuri kutoka serikalini kwa sababu lina maslahi makubwa na 
mapana kwa nchi yetu maana sasa hivi serikali inafanya mapinduzi makubwa
 katika mkoa huu ambapo inakwenda kuwekeza kwenye bandari pia tunajua 
bomba la mafuta linalotoka Hoima litakuja kuingia Tanga.
“Hayo
 yote yanaonyesha kwamba tutakuwa na shughuli nyingi za kiuchumi lakini 
tunahitaji kuwatayarisha watu wetu ili waweze kushiriki katika kutumia 
fursa hizo na maendeleo ya mkoa wa Tanga na Tanga ikiendelea inachangia 
kwenye maendeleo yetu,” alisema Profesa Kusihika.
Awali,
 Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Adam Malima alisema wamefanya mazungumzo na 
uongozi wa kujua wanafanya lakini fedha zimeshatoka kwa ajili ya 
kuanzisha chuo kikuu hicho mkoani hapa.
“Tulichokunaliana
 ni kwamba mwezi ujao Julai hadi Agosti, tutaanzisha Chuo Kikuu cha 
Mzumbe hapa Tanga kwenye maeneo ya makazi ya muda wakati tunafanya 
ujenzi wa makazi ya kudumu kwa sababu kuna maeneo matatu Mkinga, Muheza 
na Tanga.
“Tulikuwa 
tunajadiliana maeneo kwa sababu mwanzo ilikuwa fikra kwamba lipatikane 
eneo la ekari kama 200 lakini ukipata ekari 200 leo baada ya miaka 20 
utahitaji eneo la ekari 300-400 huna sehemu ya kupanua Tukasema hapana 
ndiyo maana nimewaita wakuu wangu wa wilaya wa maeneo hayo, Mstahiki 
Meya, Katibu Tawala na Ofisa Elimu wa Mkoa kwa sababu ni jambo ambalo 
kimkakati kwa masaa haya yanayokuja tunataka tupate eneo ambalo wote 
hapa tutaliangalia kwa pamoja,” alisema Malima.
Pamoja
 na mambo mengine, Malima alisema walikuwa na mkutano na Katibu Mkuu wa 
Mifugo wakakubaliana kutakuwa na Kitivo cha Mifugo ili kuendana na 
mahitaji ya mifugo, Kitivo cha Mambo ya Uchumi wa Buluu na mambo mengi 
ambayo bado wanawaza ili chuo kiwe kinafundisha masomo mahsusi ambayo 
yanaendana na mahitaji ya kanda hiyo na maeneo mengine ya Tanzania kwa 
ujumla.
“Tumekuwa na mkutano
 mzuri ambao tunaamini kwa maamuzi haya Tanga sasa itapata chuo kikuu na
 fikra ni kwamba baada ya miaka 10 kiwe ni chuo kikuu kinachojitegemea.
“Tunawashukuru
 uongozi kwa kutufikiria sisi Tanga kwanza kama ni sehemu ya kuja kuweka
 tawi lao nataka niwahakikishie Wanatanga kuwa huenda mwaka huu au 
mwakani tutakuwa kwenye makazi ya muda miaka miwili tutakuwa kwenye eneo
 mahsusi,” alisema.




Post A Comment: