Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Meru Mwl.Zainabu Makwinya ameishukuru Serikali ya awamu ya Sita chini ya Uongozi wa Rais.Samia Suluhu Hassan kwa kutoa komputa mpakato kwa  Maafisa Elimu Kata 26 wa Halmashauri ya wilaya ya Meru ambapo  amewataka  Maafisa elimu  hao kutunza na kutumia komputa hizo kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi mkubwa.


Makwinya amesema hayo wakati wa hafla ndogo ya kukabidhi laptop hizo kwa waratibu  ambapo, pia ametoa wito kwa wadau  kuwezesha upatikanaji wa chaji za nishati ya jua (solar)kwenye shule ambazo hazina nishati ya  umeme  .


Akitoa taarifa ya Komputa hizo Mwl. Marcus  Nazi ambaye ni Mkuu wa Idara ya  Elimu Awali na Msingi  amesema Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI) kupitia mradi wa LANES  II, imetoa  komputa 26 kwa Maafisa  Elimu  kata  26 za Halmashauri hiyo ambayo ni miongoni mwa Halmashauri  20  zilizonufaika na komputa kati ya Halmasauri 185 za Tanzania bara. 


Kwa upande wake Mhe.Jeremia Kishili M/Kiti wa Halmashauri ya wilaya ya Meru ameipongeza Serikali ya awamu ya Sita kwa kutoa vitendea kazi hivyo,pia kumekuwa na mwamko mkubwa wa  shughuli za Maendeleo ndani ya Halmashauri .


Afisa Elimu Kata,Kata  ya  Shambarai Burka mwl. Regina Lekule kwa niaba ya Maafisa  Elimu Kata wengine ameishukuru Serikali kwa kuwapa komputa hizo kwani awali ilikuwa ni changamoto kubwa  katika uandaaji na uwasilishaji wa taarifa  kwa wakati na kwa usahihi .


Ikumbukwe .Halmashauri ya Wilaya ya Meru inakata 26 zenye shule za Msingi 180,kati ya Shule hizo shule 116 ni shule za Serikali na Shule 64 ni shule binafsi.



Share To:

Post A Comment: