Kituo cha Afya Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo Katika Halmashauri ya Korogwe Mkoani Tanga(Picha zote na Yusuph Mussa)
Mwanamke Amina Kea wa Kijiji cha Mkata Magharibi Kata ya Mkata Tarafa ya Mazingara wilayani Handeni akifurahia baada ya kujifungua mtoto wa kiume February 26,2022 na kupewa jina la Abdulrahman"Putin" katika Kituo cha Afya Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe mkoani Tanga Barabara Kuu ya Korogwe -Handeni (Picha na Yusuph Mussa)
Muuguzi wa Kituo cha Afya Zayu Kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halamshauri ya Mji wa Korogwe barabara kuu ya Korogwe-Handeni Hilda Singano akimpima uzito mtoto wa miezi sita (Picha na Yusuph Mussa)
MKURUGENZI Mtendaji Msaidizi wa Kituo cha Afya Zayu Kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mkoani Tanga Barabara kuu ya Korogwe-Handeni Jamilah Masoud akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maendeleo na mipango ya kituo hicho(Picha na Yusuph Mussa)
Mtaalamu wa Maabara kituo cha Afya Zayu Kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe barabara kuu ya Korogwe-Handeni Peter Msuva akiwa kazini(Yusuph Mussa)
Kituo cha Afya Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halamshauri ya Mji wa Korogwe barabara kuu ya Korogwe-Handeni kulia ni Jengo la Utawala,vyumba vya madaktari,wodi za kawaida na huduma nyengine na kushoto ni wodi ya VIP (Yusuph Mussa)
NA YUSUPH MUSSA,KOROGWE
Mwanamke Amina Kea wa Kijiji cha Mkata Magharibi Kata ya Mkata Tarafa ya Mazingara wilayani Handeni akifurahia baada ya kujifungua mtoto wa kiume February 26,2022 na kupewa jina la Abdulrahman"Putin" katika Kituo cha Afya Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe mkoani Tanga Barabara Kuu ya Korogwe -Handeni (Picha na Yusuph Mussa)
Muuguzi wa Kituo cha Afya Zayu Kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halamshauri ya Mji wa Korogwe barabara kuu ya Korogwe-Handeni Hilda Singano akimpima uzito mtoto wa miezi sita (Picha na Yusuph Mussa)
MKURUGENZI Mtendaji Msaidizi wa Kituo cha Afya Zayu Kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mkoani Tanga Barabara kuu ya Korogwe-Handeni Jamilah Masoud akizungumza na waandishi wa habari kuhusu maendeleo na mipango ya kituo hicho(Picha na Yusuph Mussa)
Mtaalamu wa Maabara kituo cha Afya Zayu Kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe barabara kuu ya Korogwe-Handeni Peter Msuva akiwa kazini(Yusuph Mussa)
Kituo cha Afya Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halamshauri ya Mji wa Korogwe barabara kuu ya Korogwe-Handeni kulia ni Jengo la Utawala,vyumba vya madaktari,wodi za kawaida na huduma nyengine na kushoto ni wodi ya VIP (Yusuph Mussa)
GARI la kubabea wagonjwa kituo cha Afya Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo katika Halmashauri ya Mji wa Korogwe Mkoani Tanga (Picha na Yusuph Mussa) |
NA YUSUPH MUSSA,KOROGWE
WANANCHI
zaidi ya 500 katika Halmashauri ya Mji Korogwe mkoani Tanga wamefaidika
na upimaji wa bure wa afya zao kwenye zoezi lililofanywa na Kituo cha
Afya cha Zayu kilichopo Kata ya Bagamoyo mjini Korogwe.
Katika
zoezi hilo, wananchi saba walikutwa na ugonjwa wa ngirimaji (busha),
watatu walikuwa na ugonjwa wa henia na mmoja kidole tumbo, na wote
walifanyiwa upasuaji papo hapo. Lakini wanawake sita walikutwa na dalili
za saratani ya shingo ya kizazi.
Hayo
yalisemwa (Feb. 28) na Shara Harith ambaye ni Tabibu wa Kituo cha
Afya Zayu, na kuongeza kuwa katika upimaji huo, wanawake wawili
walikutwa na viashiria vya saratani ya shingo ya kizazi.
"Baada
ya kuona wananchi hawana utamaduni wa kupima afya zao mpaka waumwe,
kituo chetu kina utaratibu wa kupima afya bure kwa wananchi ambao wengi
wao wanapata huduma kwetu. Katika zoezi hili tumeweza kupima wananchi
340, ambapo kati yao, saba walikutwa na ngirimaji, watatu walikuwa na
henia, mmoja kidole tumbo na wanawake wawili walikutwa na viashiria vya
saratani ya shingo ya kizazi" alisema Harith.
Harith
alisema zoezi kama hilo pia walilifanya Septemba, 2020, ambapo zoezi
hilo lililenga kuwapima wanawake saratani ya shingo ya kizazi, ambapo
wanawake 255 walijitokeza, na kati yao sita walikutwa na dalili za
saratani hiyo, na waliweza kuwasaidia kwa kuwasafirisha bure kwa gari la
wagonjwa wa kituo hicho kwenda Hospitali ya Rufaa ya Bombo, Tanga.
"Tunapofanya
mazoezi haya ya upimaji, tunawashirikisha madaktari bingwa kutoka
Hospitali ya Wilaya ya Korogwe, Magunga. Tunawapima afya yao, na
tunapowakuta na kesi mbalimbali, wengine tunawafanyia upasuaji hapa hapa
kwenye kituo chetu cha afya kwa kiwango kidogo cha fedha, na wale wenye
changamoto kubwa, tunawasafirisha kwa gharama zetu kwa kutumia gari
letu la wagonjwa kwenda Hospitali ya Bombo" alisema Harith.
Harith
alisema ujio wa Bima ya Afya ya NHIF Septemba, mwaka jana, imeongeza
nguvu katika utoaji huduma kwenye kituo hicho cha afya, kwani pamoja na
huduma nzuri waliyokuwa wanatoa kwa jamii, Bima ya Afya ilikuwa kikwazo,
kwani baadhi ya watumishi wa Serikali, Sekta Binafsi na mtu mmoja mmoja
ambao walikuwa na bima hiyo, walishindwa kupata huduma kwenye kituo
hicho cha afya.
"Tumeanza
kutoa huduma kupitia Bima ya Afya ya NHIF Septemba, mwaka 2021. Na hiyo
itarahisisha utoaji huduma kwa watumishi wa Serikali, Sekta Binafsi na
baadhi ya makundi yanayotumia bima kwenye jamii. Malengo yetu ni
kusogeza huduma kwa wananchi ikiwa ni pamoja na mazoezi ya upimaji afya
kwa wananchi mara kwa mara ili kuwaibua watu wenye shida mbalimbali
kupata tiba kwa wakati, kusaidiana na Serikali kutoa huduma za afya, na
kuongeza majengo mengine ya wodi za wagonjwa" alisema Harith.
Naye
Mkurugenzi Mtendaji Msaidizi wa Kituo cha Afya cha Zayu, Jamilah
Masoud, alisema wanaishukuru Serikali ya Awamu ya Sita ya Rais Samia
Suluhu Hassan, kwani imetoa wigo mpana kwa taasisi binafsi ikiwemo Sekta
ya Afya kuchangia kutoa huduma kwa wananchi, na ndiyo maana na wao
wamevutiwa kusaidia jamii kwa kufanya zoezi la upimaji afya bure.
"Tunamshukuru
Rais Samia Suluhu Hassan kwa kuonesha kuunga mkono Sekta Binafsi katika
kufanya shughuli za kuhudumia jamii pamoja ikiwemo Sekta ya Afya. Sisi
tumekuwa tukiendesha mazoezi ya kuwapima afya bure wananchi, na wale
wanaokutwa na matatizo, tunawafanyia upasuaji kwa gharama nafuu. Lakini
na wale wanaohitaji rufaa, tunawapeleka kwa gharama zetu kwa kutumia
gari la Kituo cha Afya Zayu" alisema Masoud.
MWISHO.
Post A Comment: