Taasisi ya Bega kwa Bega na Mama Samia Suluhu Hassan kwa kushirikiana na akina mama wilaya ya Shinyanga Mjini wameandaa sherehe Maalumu ya Maadhimisho ya mwaka mmoja wa Mhe. Rais Mama Samia Suluhu Hassan madarakani. Sherehe hizi zitafanyika Mjini Shinyanga Machi 12 - 13 2022.

Katika Sherehe hizo Taasisi ya Bega kwa Bega na Mama Samia Suluhu Hassan imeandaa Matembezi Maalumu siku ya Jumamosi Machi 12,2022 yatakayoanzia Viwanja vya CCM Mkoa wa Shinyanga mpaka uwanja wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga.

👉 Vile vile Taasisi hiyo imeandaa Semina kwa Wajasiriamali wadogo wadogo na Wamachinga, siku ya Jumapili Machi 13,2022 katika ukumbi wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini, watapewa Elimu juu ya umuhimu wa kupata Bima za Moto ili kulinda Mitaji yao na Majanga ya moto.
Share To:

Post A Comment: