NA HERI SHAABAN


JUMUIYA ya Wazazi Wilaya ya Ilala imetoa onyo kwa makatibu na Wenyeviti ngazi ya Kata na Matawi wasimamie Uchaguzi vizuri bila kukata majina.


Agizo hilo limetolewa katika ziara ya Kamati ya Utekelezaji Wilaya llala na Mwenyekiti wa Wazazi Wilaya llala, MOHAMED MSOPHE, wakati wa mkutano wa wanachama ukumbi wa mikutano check pont Ukonga wakati wa kutoa elimu ya Sensa ya makazi, Kuhamashisha wanachama kujisajili katika mfumo wa kielectronik pamoja na elimu ya korona na Uchaguzi ndani ya chama.


Mwenyekiti MSOPHE alisema kila mtu anayo haki ya kugombea ndani ya Jumuiya ya wazazi hivyo makatibu wa Kata na Matawi isiwe chanzo Cha  malalamiko ya kukata majina yakapelekea kuvuruga Uchaguzi wa wazazi.


"Nawaomba WENYEVITI kutenda haki kusimamia uchaguzi wa tawi vizuri mrudishe majina msikate majina  bila sababu za Msingi" alisema Msophe.


  Msophe alisema uongozi unapangwa na Mungu kila mtu anayo haki ya kugombea uongozi anaoitaji  Wananchi ndio watamuukumu.


Aidha Mwenyekiti Msophe aliwamasisha wanachama wa Jumuiya ya Wazazi kujisajili katika mfumo wa kielectronik kadi za Jumuiya ya Wazazi Ili waweze kushiriki kupiga kura.


Aliwataka wajenge Jumuiya ya Wazazi vizuri na kuweka mikakati mbalimbali ikiwemo kubuni miradi ya Jumuiya .


Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wazazi Wilaya SHAMSUDN HEMED alizungumzia elimu ya Sensa ya makazi akiwataka makatibu wa Jumuiya hiyo na Wanachama kutoa elimu hiyo na kuwa BALOZI wa mwezake Wananchi washiriki sensa kwa Maendeleo ya Taifa.


Kwa upande wake Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji Wilaya Miraji Kibuba  ametoa agizo  kwa MAKATIBU Tawi MAKATIBU kata na Kamati za Utekelezaji wasim ame wenyewe  kutoa fomu katika uchaguzi wao.


Kibuba alitoa onyo wasipange safi katika Uchaguzi wa wazazi wakapatikana viongozi si sahihi ndani ya Jumuiya hiyo.


Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: