Balozi wa kodi TRA Bw. Edward kumwembe akifanya zoezi la hakiki stamp. Balozi wa kodi TRA Bw. Edward kumwembe akitoa elimu ya hakiki stempu Mkoani manyara.Afisa wa TRA Bw. Chama Siriwa akitoa elimu ya kodi 

***************** 

Wafanyabiashara wa Vinywaji pamoja na watumiaji wametakiwa kuwa na utaratibu wa kuhakiki Vinywaji kwa kutumia app maalumu ya Hakiki stempu ili kutambuwa bidhaa feki sokoni ambayo zinaweza kuleta athari kwa mlaji. 

Akizungumza mjini Babati Mkoani Manyara Balozi wa Kodi Edward Kumwembe amesema application ya Hakiki stempu inauwezo wa kutambua uhalali wa bidhaa za Vinywaji ambazo zipo sokoni ambapo mtumiaji atapaswa kuwa na Application hiyo katika simu janja na kufanya uhakiki kwa kutumia simu yake kama iwapo bidhaa hiyo inafaa kwa matumizi ya binadamu. 

Kumwembe amesema "kuna app maalumu ambayo inapatikana katika hizi simu za smartphone ambazo Zina application au maarufu watu wanaita App ambayo inahakiki ubora wa Vinywaji vyako, ambayo inahakiki kwa njia mbili wewe ukiwa ni mnunuaji kutoka sehemu nyingine unaweza inahakiki Vinywaji vyako lakini vilevilie wewe unapomuuzia mtu mwingine mteja naye anaweza kuhakiki kwasababu wakati mwingine unaweza kununua kitu ambacho hakina ubora lakini siyo kosa lako" . 

Aidha Kumwembe amesema lengo la kuhakiki ubora wa bidhaa za Vinywaji ni kwa sababu kuna aina nyingi za Vinywaji hivyo siyo rahisi kufahamu ubora wa Vinywaji hivyo. 

Amesema kwa kutumia mfumo huo wa app utaweza kupata taarifa sahihi kuhusu ilipotoka bidhaa,ilipotengenezwa,na lini itaisha muda wake wa matumizi hivyo kumfanya mlaji wa bidhaa husika kuwa salama. 

Kwa Upande wake muuzaji wa Vinywaji mbalimbali kutoka Mjini Babati Bw.Naingwa ameishukuru mamlaka ya Mapato Tanzania kwa kutoa elimu juu ya matumizi sahihi ya kutumia application hiyo inayoweza kuhakiki ubora na uhalali wa Vinywaji na kwamba itawasaidia kuepuka kununua bidhaa feki. 

"Application hii inafaida nyingi kwa sisi wafanyabiashara hasa pale tunapo kwenda kununua Vinywaji kwani itatusaidia kutambuwa Vinywaji feki pamoja na kufahamu ubora wa Vinywaji hivyo ili kumlinda mteja"alisema. 

Hata hivyo maafisa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kutoka Makao Makuu wapo Mkoani Manyara kwa siku kumi katika kampeni ya walioiita Mlango kwa mlango (Door to door) inayolenga kutoa elimu kwa Wananchi na wafanyabiashara juu ya matumizi sahihi ya EFD machine,matumizi ya Hakiki stempu inayolenga kutambuwa Vinywaji feki sokoni na msisitizo wa kutoa na kudai risiti baada ya kuuza au kununua bidhaa.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: