Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula,akizungumza katika kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.Kulia ni Mkurugenzi wa idara ya Sera na Mipango Wizara ya Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Bw.Sayi Magessa


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula,akielezea jambo kwa washiriki wakati wa kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula,akimsikiliza Mkurugenzi wa idara ya Sera na Mipango Wizara ya Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Bw.Sayi Magessa wakati akielezea lengo la kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.


Sehemu ya washiriki wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula (hayupo pichani) wakati wa kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.


Mratibu wa Mradi wa majaribio wa kukabiliana ba udhalilishaji na unyanyasaji wa watoto,akizungumza na waandishi wa habari mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.


Naibu Mkurugenzi wa shirika la wanawake katika sheria na maendeleo barani Afrika Bi.Cecilia Assey,akielezea mikakati ya shirika hilo wakati wa kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.


Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula,akiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kumalizika kwa kikao cha kamati tendaji ya taarifa ya utekelezaji wa mpango kazi wa taifa wa kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto (MTAKUWA) kwa kipindi cha Julai hadi Desemba 2021 kilichofanyika jijini Dodoma.

..........................................................

Na.Alex Sonna,DODOMA

Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula amewataka watendaji wa Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na watoto (MTAKUWWA) kubadilika na kufanya kazi kwa matokeo.

Dkt. Chaula ameyasema hayo jijini Dodoma wakati akifungua kikao cha Kamati tendaji inayojumuisha Idara na Wizara zinazotekeleza Mpango huo.

Dkt. Chaula amesema kila mmoja anayehusika na kutekeleza Mpango huo atekeleze majukumu aliyopewa na matokeo yawe ya takwimu ili kiwe na uhalisia.

Amesema lazima kuwe na vigezo vya kuondoa changamoto za ukatili zilizopo ili matokeo yaonekane kuanzia ngazi ya vijiji na Mitaa.

"Utendaji wetu wa kazi uwe na matokeo, mpango huu wa miaka mitano kila mmoja atekeleze wajibu wake na kazi yoyote uliyopewa lazima iwe na matokeo kwa takwimu" alisema Dkt. Chaula

Ameongeza kuwa kama Kamati ikitekeleza majukumu yake, vitendo vya ukatili vitapungua na havitatokea katika jamii zetu.

Kwa upande wake Geoffrey Chambua mratibu wa mradi wa majaribio kutokomeza ukatili wa kingono amebainisha kuwa katika mradi huo uliofanyika kwa miezi mitatu Wilaya ya Kinondoni ilionekana kuna umuhimu wa kuwa na vituo vya mkono kwa mkono vinavyowasaidia waathirika wa ukatili wa kingono kupata huduma muhimu kwa pamoja na kwa wakati.

Naye Naibu Mkurugenzi wa shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo WILDAF Cesilia Assey, ameipongeza Serikali kwa kushirikiana na Wadau wa Maendeleo kwa karibu na kutoa wito kwa wadau wote kushirikiana kutokomeza tatizo la ukatili.

Aidha amesema lengo ni kufikia hatua ya huduma kwa waathirika wa ukatili zinapatikana kwa urahisi na wananchi wanafikiwa kupata elimu kuhusu madhara ya ukatili katika Jamii.
Share To:

emmanuel mbatilo

Post A Comment: