Julieth Ngarabali.Pwani.


Naibu Waziri wa Wizara ya Ardhi,nyumba na maendeleo ya makazi  Ridhiwan Kikwete  amesema Serikali  imetoa muda wa siku 60 kuanzia  Februari 05  mwaka huu kuhakikisha wale wote waliopimiwa viwanja wanawasilisha maombi ya kumilikishwa.


Amesema kwa wale wananchi wenye milki za ardhi  nao pia wanatakiwa wawe wamelipa kodi ya pango la ardhi  ndani ya muda huo uliyotolewa.


"Mmiliki ambaye hatalipa kodi ndani ya muda uliotolewa,Serikali itachukua hatua kisheria ikiwemo kufuta umiliki,kupiga mnada na kumilikisha viwanja vilivyopimwa kwa wananchi wengine wenye uhitaji "amesema Ridhiwan


Ridhiwan ambaye pia ni Mbunge wa Chalinze  amebainisha  kuwa zoezi  la kuchukua sheria dhidi ya wasiolipa kodi  litaanza rasmi  Aprili 04 (nne) mwaka huu 


Naibu Waziri huyo ameongeza kuwa Wizara   yake kwa sasa inakumbusha Umma kwamba ni wajibu wa kisheria kwa wale ambao ardhi zao zimepangwa na kupimwa kuwasilisha maombi ya kumilikisha ardhi kwa Kamishna wa ardhi kwa ajili ya kumilikishwa.

Share To:

Post A Comment: