MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) kupitia Kundi la Asasi za Kiraia Tanzania (NGOs) Neema Lugangira akizungumza wakati wa kikao hicho

Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wanawake  na Makundi Maalumu Dkt. Dorothy Gwajima akizungumza wakati akifungua kikao hicho
Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. Zainab Chaula akizungumza wakati wa kikao hicho

Sehemu ya washiriki wa kikao hicho

NA MWANDISHI WETU, DODOMA.


MBUNGE wa Viti Maalumu (CCM) kupitia Kundi la Asasi za Kiraia Tanzania Bata (NGOs) Neema Lugangira ameshiriki kikao kazi cha Wadau kwa ajili ya kuweka Mkakati wa kuimarisha Utekelezaji wa Afua za Kutokomeza Ukatili wa Dhidi ya Wanawake na Watoto - MTAKUWWA

Kikao hicho ambacho kilifanyika Jijini Dodoma na kilihudhuriwa na wadau mbalimbali na kufunguliwa na Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wanawake  na Makundi Maalumu Mhe Dkt. Dorothy Gwajima ambapo Mbunge Lugangira aliziomba Mamlaka husika kuhakikisha Eimu ya Ukatili wa Kijinsia inafika kwa Jamii nzima.

Ikiwemo kuangaliwa kwa umakini kuhakikisha Vyumba vya Madawati ya Kijinsia visiwe ndani ya Jengo la Polisi badala yake kuandaliwe utaratibu mzuri ambao utakuwa ni rahisi kwa wananchi kuweza kufikia kwenye maeneo hayo maana hivi sasa ni ngumu sana kwa mtu aliyefanyiwa Ukatili wa Kijinsia au Mzazi wa Mtoto akiyefanyiwa Vitendo vya Ukatili wa Kijinsi kupokelewa Polisi na mbele ya kila mtu aeleze shida yake alafu aingie ndani ya Polisi apelekwe chumba chenye Dawati la Kijinsia, haya sio mazingira rafiki.

 Akizungumza wakati wa kikao hicho Mbunge Neema alisema ni muhimu pia MTAKUWWA itambue kwamba Ukatili wa Kiinsia Mtandaoni unavyopelekea kuwafanya Vijana wa Kike, Wanawake na hata Viongozi Wanawake wakiwemo Wanasiasa Wanawake washindwa kutumia Mitandao ya Kijamii ipasavyo kwa kujiepusha na Ukatili huo.

Alisema wakati umefika MTAKUWWA itambue pia Masuala ya Afya ya Akili na hilo ni  jambo la kudharura kwa kuzingatia matukio mengi ya ukatili wa Kijinsia ambayo ni katika ya visababishi ni pamoja na Msongo wa Mawazo . 

Awali akizungumza wakati akitoa hotuba yake Waziri wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii,Jinsia ,Wanawake na Makundi Maalumu Mhe Dkt. Dorothy Gwajima alikubaliana na Ushauri wa Mbunge Lugangira hivyo kuelekeza Wizara na Wadau washirikiane katika kuimarisha maeneo haya muhimu yaliyoainishwa na Mhe Neema Lugangira.

Share To:

TANGA RAHA BLOG

Post A Comment: