Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akikabidhiwa zawadi na Rais wa chuo kikuu cha Iringa (Tumaini) Elius wiliam baada ya kufika chuoni hapo kwa mara ya kwanza.
Mkuu wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo akiongea na baadhi ya wanafunzi wa chuo kikuu cha Iringa juu ya kuachana na biashara ya ngono na wafuate kilichowapeleka chuoni.
Na Fredy Mgunda,Iringa.
MKUU wa Wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo alisema tabia ya
baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu mkoani Iringa Kujihusisha na Biashara ya
Ngono kunadharirisha Utu na hadhi ya Vyuo,elimu wanayoipata na hilo sio kusudio
la serikali.
Akizungumza wakati wa hafla ya kuwakaribisha wanafunzi wa mwaka
wa kwanza wa chuo Kikuu Iringa (Tumaini) alisema Serikali imebaini kuwapo kwa
wasichana wanaofanya biashara hiyo haramu huku akionya kuchukua hatua.
Moyo alisema kuwa serikali inawategemea wasomi wa Elinu ya juu
kuwa chachu ya maendeleo kwa kufanya tafiti zenye tija na kuishauri serikali Juu
ya masuala ya maendeleo, na si kujihusisha na vitendo vya aibu
Alisema kuwa tatbia hiyo inachafua taswira ya elimu ambayo
inatolewa na vyuo vikuu vya mkoani Iringa kwasbabu ya wanafunzi wachache ambao
wamejikita katika biashara hiyo ya ngono.
Moyo alionyesha kukerwa na vitendo vya baadhi ya wanachuo kwa
tabia zao za kujihusisha na biasha ya Ngono lakini anavitaja vitendo hivyo
vinaondosha thamani ama hadhi ya elimu ya vyuo vikuu na kuchafua taswra halisi
ya elimu hiyo ya juu
“Ukipita kwenye kumbi mbalimbali za starehe nyakati hasa za siku
unakutana na wimbi kubwa la baadhi ya wanafunzi wa vyuo vikuu wapo wanadanga tu
bila sababu yoyote ya msingi hivyo wanafunzi wanatakiwa kuacha mara moja tabia
hiyo ya udangaji” alisema
Alisisitiza kwa wanafunzi wa elimu ya juu wanaosoma vyuo
vilivyopo mkoani Iringa kuachana na tabia zisizo na tija na badala yake sasa
wajielekeze katika uzalendo wa kweli kwa Taifa.
Moyo alisema kuwa serikali imekuwa inatoa mikopo kwa wanafunzi
wa vyuo vikuu kwa lengo la kuwasaidia kutimiza majukumu yao yaliyowapeleka
vyuoni na sio fedha hiyo waitumie kwenye starehe kama ambavyo baadhi yao
wamekuwa wakifanya.
Alilazimika kuyasema hayo kutokana na baadhi ya wanasiasa na
wanaharakati kuwatumia vijana wa vyuo vikuu nchini kuichafua serikali kwa
kuwakashifu viongozi waliopo madarakani na kupinga masuala ya maendeleo pasipo
kupima athari zinazoweza kujitokeza kwa Taifa
Moyo alisema kuwa biashara ya ngono inamadhara makubwa kwa
wanafunzi kwa kuwa wanaweza kupata mimba na magonjwa mbalimbali ambayo
yatasababisha kutisha ndoto zao za kupata elimu ya juu.
Kwa upande wake rais wa chuo kikuu cha Iringa (tumaini) Elius
wiliam alisema kuwa wataendelea kutoa elimu kwa wanafunzi wa chuo hicho juu ya
madhara yanayotokana na biashara ya ngono ambayo baadhi ya wanafunzi wanakuwa
wanaifanya.
Wiliam aliwataka wanafunzi wa chuo hicho kuyaishi maisha ya chuo
kwa kangalia ni kilicho wapeleka kufika chuoni ili wafikie malengo ya na
akasema kuwa starehe zipo tu haziishi duniani hivyo watimize kwanza malengo
ndio wafanye mambo mengine.
Naye makamu mkuu wa chuo kikuu cha Iringa Profesa Ndelilio Urio
alimushukuru mkuu wa wilaya ya Iringa kwa kuwafunda wanafunzi hao kwa maswala
mbalimbili ikiwepo wa madhara ya bishara ya ngono kwa wanafunzi.
Post A Comment: