Wakati baadhi ya watu wakiendelea kutoa Maoni baada ya hukumu ya miaka 30 jela kwa aliyekuwa Mkuu wa wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya, mrembo ambaye ni video vixen na mjasiriamali @officiall_nai ameibuka na kumuonea huruma Mkuu huyo wa zamani wa wilaya aliyekwenda kutumikia kifungo cha miaka 30 jela.



@officiall_nai ametumia ukurasa wake wa Instagram kuonesha masikitiko yake hayo, kwa ku Share picha ya Sabaya na kuandika ujumbe unaotafsrika kwa kiswahili "hakuna mkamifu, Mungu akusimamie" huku akiweka wazi kuwa atakumbuka bata alilokuwa akipata pindi anapokwenda mkoani Arusha ,kabla ya kuifuta post hiyo.
Share To:

Teddy Kilanga

Post A Comment: