Mkuu wa mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge  akizunguza na Wananchi wa Kijiji wa Itagata hivi karibuni kuhusu umuhimu wa kilimo cha umwagiliji  na mikakati ya kurejesha skimu ya Umwagiliaji ya Itagata ambayo imegharimu kiasi sh shilingi Bilioni 2.2.

Mkuu wa Wilaya ya Manyoni   Rahabu Mwagisa (aliyesimama) akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Itagata hivi karibu. Mkutano huo ulihusu uhuishaji wa skimu ya umwagiliaji ya Itagata  ambayo serikali imetumia fedha nyingi lakini haitumuiki ipasavyo.


Baadhi ya Wananchi wa Kijiji cha Itagata wakisikiliza maagizo ya mkuu wa mkoa kuhusu uboreshaji wa skimu ya Itagata.
Mkuu wa mkoa akisikiliza kero mbalimba kutoka kwa wakulima wanaotumia skimu ya Itagata mara baada ya kumaliza mkutano wa hadhara.



Na Bashiri Salum, Itigi.


MATUMAINI ya kurejea kwa kilimo cha umwagiliaji katika skimu ya Itagata iliyopo Wilayani Itigi Mkoani Singida yameanza kujitokeza  kwa Wakulima baada ya kuanza kutekelezwa kwa  maagizo ya Mkuu wa Mkoa wa Singida Dkt. Binilith Mahenge ya kuvunja uongozi uliokuwepo na  kuchukuliwa kwa mashamba ambayo hayaendelezwi katika skimu hiyo.

Ikiwa ni mwezi mmoja umepita  baada ya mkuu wa mkoa kutembelea skimu hiyo na kuwataka wakulima kuchagua uongozi mpya ambao  utashirikiana na viongozi mbalimbali kufanya tathmini ya ugawaji na uendelezaji wa mashamaba, jana Oktober 23, 2021 kwa mara nyingine ametembelea skimu hiyo na kukuta wamechagua viongozi wapya  na tathmini ya mashamba  imefanyika.

Akizungumza wakati wa mkutano wa hadhara na wakulima hao Mahenge amemshukuru mkuu wa  wilaya hiyo Rahabu Magesa na viongozi wengine kwa kuanza kutekeleza maagizo yake na kuwaeleza kwamba  hatua hiyo  iwe endelevu na kuhakikisha wakulima wanafuata sheria na taratibu za skimu hiyo.

“Skimu hiyo iligharimu kiasi cha shilingi bilioni 2.2 tokea ilipoanza kujengwa mpaka mwaka 2019 ilipokabidhiwa kwa kijiji husika, ni lazima lazima usimamizi ufanyike ili uzalishaji uongeze iweze kutoa mchango kwa taifa” alikaririwa Dkt. Mahenge.

Aidha Dkt. Mahenge akiwa kijijini hapa akatoa wito kwa wakulima wote  wenye umiliki wa mashamba katika skimu hiyo kulipa ada zinazotakiwa ambazo zitatumika kukarabati miuondombinu ya skimu pale itakapo hitajika.

Hata hivyo Rc huyo alisema ulinzi wa miundombinu ya  skimu ni jukumu la kila mwananchi hivyo akawakumbusha watu wenye makazi ndani ya Skimu kuhakikisha wanafuata sheria zilizowekwa kwenye skimu hiyo kama wakishindwa watalazimika kuhama.

Aidha maagizo hayo yametokana na malalamiko yaliyowasilishwa na Afisa Kilimo kwamba wakazi hao wamekuwa wakiwatishia wakulima wengine wakidai eneo hilo lipo chini yao jambo ambalo limeleta kero kwa wakulima wengine.

Akijibu maswali ya wananchi ambao wametakiwa kulipia ada wakati mashamba yao hayajafikiwa na miundombinu ya umwagiliaji na kufanya kilimo chao kutengemea mvua za msimu Mahenge akaendelea kutoa maelekezo kwa Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo kuhakikisha miundombinu inatengenezwa maeneo yenye changamoto ya kufikisha maji ili wakulima waweze kumwagilia .

“Nataka tuelewane kwamba kila mkulima ndani ya skimu anahaki sawa na mkulima mwingine hivyo kila mtu anatakiwa kufikiwa na maji na kutoa ada kulingana na ukubwa wa anachokimiliki”.aliendelea kufafanua Mahenge.

DC wa wilaya hiyo Rahabu Mwagisa alisma kwa sasa wakulima hao wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa mitaji ila serikali inaendelea kuwaunganisha na wadau mbalimbali zikiwemo taasisi za kifeza ili kupata mikopo  

Rahabu akawashauri  wakulima hao kulima mpunga kwa kuwa soko lake ni la uhakika na watakao amua kulima matunda au mbogamboga wahakikishe wanalima kwa wingi kwa ajili ya kulitosheleza soko.

Awali Afisa kilimo wa kijiji cha Itagata  Bi. Halima Issingo alibainisha kwamba skimu hiyo ina ukubwa wa ekari 400 zinazofaa kwa kilimo na inauwezo wa kulisha wilaya nzima endapo itafanya kazi kwa viwango vyake vyote.

Afisa kilimo huyo alisema  jumla ya ekari 209 kati ya 400 zimegawiwa kwa wanachama  na kati hizo ekari 115 ndizo zililzolimwa mpunga  na kutoa tani 120.75 wakati ekari 26 zililimwa mahindi na kutoa tani 14.4

Alisema moja ya mipango ndani ya skimu ni kufikisha miundombinu ya umwagiliaji katika maeneo ambayo hayana ili kuifanya skimu nzima iweze kuzalisha vya kutosha.

Wakulima nao wakapata nafasi ya kutoa maoni baada ya mkutano ambapo Musa Saidi mkulima wa skimu hiyo wameishukuru serikali kwa hatua walioichukua ya kuhuisha skimu hiyo na kuomba wataalamu waendelee kutoa elimu kwa wakulima ili kubadilisha mazingira ya uzalishaji na kulima ki biashara.

Michaeli Simuli Ngawe mkulima wa mpunga naye akiomba  serikali kuwaletea mbolea na mbegu za kisasa za mpunga  kwa kuwa wengi wao hawatumii mbolea na mbegu bora kwa kuwa dhamiara ya serikali na wakulima kwa sasa ni kubadilisha kilimo kiwe chenye tija.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: