Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof.James Mdoe akizungumza na wajasiriamali waliopatiwa mafunzo na  Shirika la kuhudumia Viwanda Vidogo  (SIDO) ya kukuza ujuzi kupitia mradi wa kuongeza na kukuza ujuzi kwa Vijana na wanawake katika ziara yake ya kukagua utekelezaji wa mradi huo.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Elimu Tanzania Bahati Geuzye akizungumza kwenye ukaguzi huo.

Meneja wa Shirika la kuhudumia Viwanda vidogo (SIDO) Mkoa wa Singida Agnes Yesaya akizungumza kwenye ukaguzi huo.

Mjasiriamali Happy Francis akichangia jambo kwenye ukaguzi huo.

Afisa Mafunzo na Masoko kutoka SIDO  Singida,  Joel Tangai akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof.Mdoe, Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Geuzye na Viongozi wengine wakisikiliza taarifa fupi ya Mradi kutoka SIDO

Wajasiriamali wakionesha bidhaa zao wanazozizalisha baada ya kupatiwa mafunzo ya kukuza ujuzi na SIDO.

Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Prof.Mdoe akikagua bidhaa za wajasiriamali.

Ukaguzi ukiendelea.
Picha ya pamoja.
Picha ya pamoja.
 


Boniphace Jilili na Dotto Mwaibale, Singida.


NAIBU Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Profesa. James Mdoe ameliagiza Shirika la kuhudumia Viwanda vidogo (SIDO) Mkoa wa Singida kuangalia namna nyingine ya kuwawezesha mikopo wajasiriamali ili waweze kuongeza ufanisi kwenye biashara zao.

Prof.Mdoe alitoa wito huo leo alipolitembelea shirika hilo kwa lengo la kukagua utekelezaji wa mradi wa kuongeza ujuzi kwa Vijana na wanawake unaofadhiliwa na Benki ya Dunia.

Alilitaka shirika hilo kuongeza muda wa kurejesha mikopo ya wajasiriamali walionufaika na mradi huo ambao pia SIDO hutoa mkopo kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali mbalimbali kukuza biashara zao badala ya miezi mitatu iwe zaidi ya hapo.

"Ni kweli mumewapa mikopo lakini huu muda wa miezi mitatu ni mfupi angalieni namna ya kuwaongezea muda." alisema Profesa Mdoe.

Alisema Wizara ina mradi wa kuongeza ujuzi kwa Vijana na wanawake kupitia Vyuo vya Veta, chuo cha maendeleo ya jamii na mashirika ya Umma kama SIDO kwa kupatiwa mafunzo yatakayo saidia kujiajiri na kwamba unasimamiwa na Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) 

Aidha aliipongeza SIDO mkoani hapa kwa kuwawezesha wajasiriamali mbalimbali kwa kuwapatia mafunzo yatakayo wasaidia kuanzisha na kusimamia biashara wanazozianzisha ili ziwe na tija.

Alitoa wito kwa wanufaika hao kujiunga kwenye vikundi ili waweze kupata mikopo ambayo pia hutolewa na Halmashauri kuliko mtu mmoja mmoja kwani wengine hawatapata.

Akizungumzia mradi huo Mkurugenzi Mkuu Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) ambao ndio msimamizi wa mradi huo Bahati Geuzye alisema lengo la Serikali ni kuwasaidia vijana wanaoshindwa kuendelea na elimu ya juu na wanawake kukuza ujuzi ili waweze kujiajiri wenyewe.

Alisema wao kama wasimamizi wa mradi huo wanatarajia kuona vijana na watu wengine wanakuza ujuzi wao kupitia mafunzo wanayoyapata katika mashirika ya Umma na Vyuo mbalimbali vya Veta na Maendeleo ya jamii ambayo mradi umewafikia.

Kwa upande wake Meneja wa Shirika la kuhudumia Viwanda vidogo (SIDO) Mkoa wa Singida Agnes Yesaya alisema wamepokea zaidi ya milioni mia moja thelathini kwa ajili ya kuwawezesha wajasiriamali 400 lakini mpaka sasa SIDO imewawezesha wajasiriamali 436 na hadi kufikia mwisho wa mradi itakuwa imewawezesha wajasiriamali 550 zaidi ya lengo.

Mradi huo ulioanza mwaka 2019 hadi 2022 unatarajiwa kutoa matokeo chanya kwa wanawake na vijana kwa kukuza ujuzi wao hivyo kupelekea kupunguza idadi ya ukosefu wa ajira.

Share To:

dotto mwaibale

Post A Comment: