Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja Wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Ritamaty Lwabulinda  akisoma taarifa ya Mradi wa Pugu - Gongo La Mboto wenye thamani ya Bilion 7.3 uliokamilika kwa asilimia 100 na wananchi 450,000 watanufaika na mradi huo kuanzia Pugu hadi Kinyerezi.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021 Luteni Josephine Mwambashi akipata maelezo ya mradi wa Pugu - Gongo la Mboto wenye thamani ya Bilion 7.3 kutoka kwa Mkurugenzi wa Miradi na Uwekezaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Ramadhan Mtindasi walipotembelea mradi huo uliokamilika kwa asilimia 100 na kuanza kutoa huduma kwa wananchi.
Mkurugenzi wa Miradi na Uwekezaji wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) Mhandisi Ramadhan Mtindasi akifafanua jambo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa 2021 Luteni Josephine Mwambashi alipotembelea mradi wa Pugu - Gongo la Mboto uliokamilika kwa asilimia 100. Luteni Mwambashi ameridhishwa na mradi huo na kuwataka wananchi waendelee kulinda na kutunza miundo mbinu na vyanzo vya maji.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru 2021 Luteni Josephine Mwambashi akizungumza na wananchi wakati wa Kutembelea Mradi wa Pugu- Gongo la Mboto na kuwataka wananchi walinde vyanzo vya maji na miundo mbinu ya maji.

Share To:

Post A Comment: