Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi 'CCM' Daniel Chongolo akizungumza na wajumbe Secretarieti ya Taifa katika ukumbi wa Kambi ya SGR Kilosa mkoani Morogoro.


KATIBU Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi(CCM) Daniel Chongolo ameagiza ndani ya siku 14 vongozi wote wa Chama hicho na kamati zao za siasa kuanzia Mkoa na Wilaya kushuka chini kukagua miradi yote ya maendeleo inayowazunguka.

Chongolo ametoa maagizo hayo leo Agosti 10,2021 mkoani Morogoro wakati akikagua mradi wa ujenzi wa reri ya kisisasa SGR.

"Niwapongeze watu wa Morogoro kwani mmeweza kuonyesha njia nami nimeamka Nije hapa na secretarieti yangu kujionea je kinachofanyika hapa ni kile kinachoubiriwa,"amesema Chongolo na kuongeza "Haya ni maagizo na maelekezo Kama tulivyopeana mara baada ya mkutano mkuu maalum kuwa wote tushuke chini kukagua miradi ya Maendeleo katika Maeneo yetu ."

Amesema wao wanawajibu wa  kuisimamia Serikali na utekelezaji wa Ilani kwani sisi ndio tutakaorudi kuwaeleza wananchi nini tumefanya

Kwa upande wake Mkurungezi Mkuu wa Shirika la Reli nchini (TRC) Masanja Kadogosa amesema anaishikuru Serikali kwa kuwapatia fedha kwa wakati kwa ajili ya kukamilisha mradi huo huku akifafanua mpaka sasa wamelipa  hati 34 kati ya 35 huku hiyo moja ambayo inalipwa muda wowote kuanzia sasa.

Wakati huo huo  Mkuu wa Mkoa wa Morogoro,Martin Shegela  amesema uongozi wa mkoa huo umeridhishwa na kasi ya ujenzi kwani waliweza kutembelea eneo la kuanzia Kilosa mpaka Morogoro Station.

Amesema kuwa mradi huo umekuwa kichocheo kikubwa Cha uchumi wa Morogoro kwani wamekuwa wakitumia malighafi na bidhaa nyingi kutoka mkoa huo.


Mkurungezi wa Shirika la Reli Tanzania,Masanja Kadogosa akitoa neno kwa ujumbe secretarieti ya CCM Taifa inayotembelea mradi wa SGR kuanzia Kilosa kuja Dar es Salaam.

Sehemu ya Daraja linalo katisha mto Mkondoa ambapo Reli ya mwendokasi inapita juu
Mkurungezi Mkuu wa Shirika la Reli Tanzania Masanja Kadogosa akitoa maelekezo kwa wajumbe wa secretarieti ya Taifa waliofika kukagua ujenzi Reli ya kisasa wa SGR










Share To:

Post A Comment: