Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe.Mary Masanja ameelezea mikakati ya kukabiliana na Wanyamapori wakali na waharibifu wanaovamia maeneo ya makazi na kusababisha adha  kwa wananchi.


Akizungumza leo na wakazi wa Wilaya  Mwanga mkoani Kilimanjaro,  Mhe. Masanja ameitaja mikakati hiyo kuwa ni pamoja na  kupanda miti kwenye maeneo yanayozunguka hifadhi, kuweka mizinga ya nyuki ambayo itasaidia kuzuia tembo kuingia katika maeneo ya Wananchi.


Katika hatua nyingine  Mhe.Masanja amewaonya  wafugaji wanaoingiza mifugo Hifadhini  kuacha tabia hiyo  mara moja  kwani ni moja ya sababu inayochochea tembo kutoka nje ya Hifadhi kwa vile Tembo hawawezi kuvumilia kuishi pamoja na ng'ombe,  Hivyo ng'ombe  wamekuwa ni  kisababishi cha  tembo kuvamia mashamba na kuleta madhara kwa wananchi.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: