Wanawake wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, wakiserebuka katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika juzi   wilayani humo.
Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo, akimkabidhi zawadi diwani pekee mwanamke wa kuchaguliwa wa Kata ya Sepuka, Halima Nyimba katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika juzi.
Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Ikungi, Haika Massawe, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Justice Kijazi akizungumza na wanawake katika kilele cha maadhimisho hayo.
Wanawake wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, wakiserebuka katika kilele cha maadhimisho hayo.
Diwani wa Kata ya Ikungi, Abel Nkuwi, akizungumza katika maadhimisho hayo.
Wanawake wakiwa  kwenye maadhimisho hayo.
Meneja wa Miradi wa TAHA, Elianchea Shang'a, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Katibu  wa Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT), Mkoa wa Singida, Edina Kuhulu, akizungumza kwenye maadhimisho hayo.
Wanawake wa Wilaya ya Ikungi mkoani Singida, wakiserebuka katika kilele cha maadhimisho hayo.
Mbunge wa Viti Maalumu (CCM) Mkoa wa Singida, Martha Gwau, akitoa mada kwenye maadhimisho hayo.
Watoa mada wakiwa  kwenye maadhimisho hayo.
 


Na Dotto Mwaibale, Singida.


HALMASHAURI  ya Wilaya ya Ikungi mkoani Singida katika kipindi cha miaka miwili na nusu imefanikiwa kutoa mikopo zaidi ya sh. milioni 200 huku wanawake wakiwa ni wanufaika wakubwa.

Hayo yamebainishwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri hiyo Justice Kijazi wakati akizungumza katika kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika juzi.

Alisema katika fedha hizo nyingi zilikopwa na wanawake hivyo alitoa rai kuwa wanawake ni warejeshaji wazuri wa mikopo kuliko  makundi mengine lakini hata katika makundi hayo ndani yake kuna wakina mama.

" Nipende kusema kuwa mikopo mingi katika halmashauri inaenda kwenye  kundi ili la wakina mama." alisema Kijazi.

Kijazi alisema lengo la mikopo hiyo ni kutaka izalishwe hivyo aliwaomba wakina  mama hao pindi wakikopeshwa waizalishe.

Aidha Kijazi alisema kwa kutambua kuwa mama yeye ni   mtunzaji wa familia na ukimuelimisha utakuwa umeelimisha familia nzima.

" Natambua kazi kubwa wanayoifanya  wakina mama kwenye kuendeleza taifa letu kwani wao ni nguzo ya jamii inayotuzunguka ni jambo moja tu tunalotakiwa kulifanya sio kuwawezesha bali ni kuwaonesha fursa za maendeleo kwa sababu wanaweza." alisema Kijazi.

Kijazi alitoa ahadi kuwa iwapo Rais Dkt.John Magufuli ataona aendelee kukaa Ikungi atakuwa nao bega kwa bega.

Mgeni rasmi katika maadhimisho hayo Mkuu wa Wilaya ya Ikungi, Edward Mpogolo akinukuu baadhi ya maneno yaliyopo kwenye biblia alisema mwanamke ni mzazi, mlezi, mlinzi, muombezi na msaidizi kama ilivyo andikwa katika kitabu cha Mwanzo 2:18 hivyo anapaswa kuthaminiwa.

Aidha Mpogolo alisema wanawake wana nguvu na uwezo mkubwa ndio maana wanaweza kugombea nafasi mbalimbali  lakini akatoa angalizo kuwa katika siasa wanavutana wenyewe mmoja akipanda ngazi na kufika juu mwingine anamvuta ashuke chini badala ya kupeana mkono.

Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Ikungi, Haika Massawe alisema jitihada za halmashauri hiyo za kumwezesha mwanamke zinaungwa mkono na wadau wa maendeleo ambapo mashirika ya kimataifa na Asasi za kiraia zimeendelea kuwawezesha wanawake.

Alisema UN Women na watekelezaji wa miradi hiyo  (Farm Africa, TAHA, Kiwohede na C-Sema) wanatekeleza mradi wa kuimarisha usawa wa kijamii kwa kuwajengea uwezo wanawake katika kilimo, umiliki wa rasilimali na kupinga ukatili wa kijinsia.

Massawe aliyataja mashirika mengine yanayounga juhudi hizo za Serikali kwa kundi hilo kuwa ni SEMA- Singida, SPRF-Singida, NODIP, OVCCT na SMCCT.

Share To:

Post A Comment: