Serikali ya Tanzania itaendelea kutoa fursa na kuwaamini zaidi wanawake na watoto wa kike katika nafasi za uongozi, siasa, masomo na katika taasisi za umma kwa kuwa siku zote wameonesha upendo, uchapakazi, uzalendo, umakini na utekelezaji uliotukuka.
 
 Ikumbukwe Serikali imetekeleza kivitendo na itaendelea kufanya hivyo kwani leo wanawake wameendelea kuvunja rekodi ya kushika nafasi kubwa za kiuongozi hapa nchini akiwemo Mama Samia Suluhu Hassan, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhandisi Zena Ahmed Said ambaye kwa sasa ni mwanamke wa kwanza kuwa Katibu Mkuu Kiongozi na Katibu wa Baraza la Mapinduzi ya Zanzibar. Tunawapenda sana wanawake na hakika mnaweza.

Kwa kuwa leo ni Machi 8, Siku ya Wanawake Duniani, kwa niaba ya Serikali tunawatakia wanawake wote wa Tanzania heri ya siku hii na waendelee kufanya  tafakuri juu ya mchango wao zaidi kwa Taifa na dunia. Tunawapenda sana

Dkt. Hassan Abbasi
Msemaji Mkuu wa Serikali.
Share To:

Post A Comment: