Diwani Baraka Simon diwani wa kata ya Olturoto kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), amechaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti, halmashauri ya Arusha, baada ya kuchaguliwa na wajumbe wa Baraza hilo, na kupata nafasi ya kuliongoza  Baraza hilo kwa kipindi cha mwaka mmoja 2019/2020.

Akitangaza motokeo ya uchaguzi huo, Mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha, Dk. Wilson Mahera, amesema kuwa kura zilizopigwa ni 33, na hakuna kura iliyoharibika, Mheshimiwa Abert Oltulele amepata kura 13 na mheshimiwa Baraka Simon, amepata kura 20.

"Kwa mamla niliyopewa ninamtangaza mheshimiwa Baraka Simon kuwa Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha kwa kipindi cha mwaka mmoja" amesema Mkurugenzi huyo.

Makamu Mwenyekiti  mheshimia Simon, amechukua nafasi hiyo baada ya kupata kura 20, na kumshinda mpinzani wake mheshimiwa Albert Oltelele, diwani wa kata ya Oloirien kutoka chama cha CHADEMA aliyepata kura 13 kati ya kura 33 zilizopigwa.

Akizungumza baada ya kuchaguliwa, Makamu Mwenyekiti huyo mpya, licha ya kuwashukuru wajumbe hao, ameahidi kufanyakazi kwa ushirikiano na wajumbe wote, kwa lengo la kuwatumikia wananchi wa halmashauri ya Arusha.

Aidha mheshimiwa Makamu Mwenyekiti, amewasihi madiwani wote kushirikiana bila kujali tofauti zao za vyama, na kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kama ilivyowasilishwa na mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli wakati wa kuingia madarakani mwaka 2015.

Hata hivyo uchaguzi huo umefanyika kulingana na Kanuni, sheria na taratibu za kuongoza Baraza la Madiwani, kila baada ya mwaka mmoja,  kuchagua Makamu Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani.




Share To:

msumbanews

Post A Comment: