Diwani Baraka Simon diwani wa kata 
ya Olturoto kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), amechaguliwa kuwa 
Makamu Mwenyekiti, halmashauri ya Arusha, baada ya kuchaguliwa na 
wajumbe wa Baraza hilo, na kupata nafasi ya kuliongoza  Baraza hilo kwa 
kipindi cha mwaka mmoja 2019/2020.
Akitangaza motokeo ya uchaguzi huo, 
Mkurugenzi mtendaji, halmashauri ya Arusha, Dk. Wilson Mahera, amesema 
kuwa kura zilizopigwa ni 33, na hakuna kura iliyoharibika, Mheshimiwa 
Abert Oltulele amepata kura 13 na mheshimiwa Baraka Simon, amepata kura 
20.
"Kwa mamla niliyopewa ninamtangaza 
mheshimiwa Baraka Simon kuwa Makamu Mwenyekiti wa halmashauri ya Arusha 
kwa kipindi cha mwaka mmoja" amesema Mkurugenzi huyo.
Makamu Mwenyekiti  mheshimia Simon, 
amechukua nafasi hiyo baada ya kupata kura 20, na kumshinda mpinzani 
wake mheshimiwa Albert Oltelele, diwani wa kata ya Oloirien kutoka chama
 cha CHADEMA aliyepata kura 13 kati ya kura 33 zilizopigwa.
Akizungumza baada ya kuchaguliwa, Makamu
 Mwenyekiti huyo mpya, licha ya kuwashukuru wajumbe hao, ameahidi 
kufanyakazi kwa ushirikiano na wajumbe wote, kwa lengo la kuwatumikia 
wananchi wa halmashauri ya Arusha.
Aidha mheshimiwa Makamu Mwenyekiti, 
amewasihi madiwani wote kushirikiana bila kujali tofauti zao za vyama, 
na kutekeleza Ilani ya Chama cha Mapinduzi kama ilivyowasilishwa na 
mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Magufuli 
wakati wa kuingia madarakani mwaka 2015.
Hata hivyo uchaguzi huo umefanyika 
kulingana na Kanuni, sheria na taratibu za kuongoza Baraza la Madiwani, 
kila baada ya mwaka mmoja,  kuchagua Makamu Mwenyekiti wa Baraza la 
Madiwani.
Post A Comment: