Mwanzilishi wa Taasisi ya Tony Elumelu, Tony Elumelu (Kushoto), akiwa katika picha ya pamoja na na mke wa Rais wa Nigeria, Aisha Buhari (katikati) na kulia ni Mwasisi Msaidizi  Dk. Awele Elumelu. Hafla ya kutangaza majina ya wajariamali 1,000 wa Afrika wataowezeshwa na Taasisi ya
TEF ilifanyika jana jijini Abuja nchini Nigeria
 Kutokana kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Tony Elumelu anayeingia, Ifeyinwa Ugochukwu, Mkurugenzi anayemaliza muda wake Parminder Vir, Balozi WA Israel nchini Nigeria,  Shimon Ben-Shoshan, Mwasisi wa Taasisi ya Tony Elumelu, Mke wa Rais wa Nigeria Aisha Buhari, Mwasisi Msaidizi wa TEF, Dk. Awele Elumelu, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya
kutangazwa kwa majina ya wajasiriamali 1,000 watakaonufaika kwa kuwezeshwa  na taasisi hiyo.
Na MWANDISHI WETU

-ABUJA, NIGERIA

WATANZANIA 52 ni miongoni mwa waliofanikiwa kushinda katika programu ya wajariamali Afrika, inayoratibiwa na na Taasisi ya Tony Elumelu ya nchini Nigeria.

Kuchaguliwa kwao sasa kunawafanya kuwa miongozi mwa wajariamali 1,000 ambao watanufaika kwa kuwezeshwa zaidi ya Sh milioni 10 ili kuimarisha biashara zao na kuzalisha ajira kwa vijana hususani kwa nchi za Afrika.

Hatua hiyo inatokana na matokeo yaliyotanganzwa mwishoni mwa wiki na Taasisi ya Tony Elumelu (TEF) ambayo ni ya Kiafrika inayoongoza kutoa ushauri na kuwawezesha wajasiriamali kutoka Afrika.

Pamoja na hali hiyo pia ilitangaza wajasiriamali wa Afrika 3,050 kutoka nchi 54 za Afrika ambao wamejiunga kwenye mzunguko wa tano wa dola za Marekani milioni 100 katika programu ya Ujasiriamali wa TEF.

Matokeo hayo yalitangazwa jijini Abuja baada ya washauri wa maendeleo kuwasilisha mchakato wa uteuzi huo, ambapo kwa mwaka huu zaidi ya watu 216,000 waliwasilisha maombi ikiwa ni ongezeko ya watu 151,000 kutoka mwaka jana.

“Takribani maombi 90,000 yaliwasilishwa na wajasiriamali wanawake ikiwa ni ongezeko la asilimia 45, hii ni ishara ya mkakati wa Taasisi hiyo kufikia usawa wa jinisia. Wajasiriamali waliochaguliwa kila moja atapokea dola za Marekani 5,000 za mitaji ambayo haitarudishwa, upatikanaji wa washauri na wiki 12 ya mafunzo ya biashara yanayohusisha moja kwa moja mahitaji ya wajasiriamali kutoka Afrika.

“Julai 26 – 27, 2019, watakusanyika kwenye Mkutano wa Biashara wa TEF, mkusanyiko mkubwa wa kila mwaka wa wajasiriamali wa Kiafrika na mazingira ya ujasiriamali katika Bara hili la Afrika

 “Kila mwaka, tunakabiliwa na kazi ngumu – kuchagua wajasiriamali 1,000 kutoka maelfu ya waliyoomba. Wajasiriamali wetu wananjaa ya kuchochoea mabadiliko. Lazima tushirikiana kuwawezesha ili kuchochea mabadiliko tunayotaka katika bara letu,” alisema muasisi wa TEF, Tony Elumelu.

Katika hotuba yake, Mke wa Rais wa Nigeria, Aisha Buhari, alipongeza jitihada za programu na kuwasisitizia wajasiriamali waliochaguliwa kuchangia maandeleo ya bara la Afrika.

“Nina imani hawa wajasiriamali wa Tony Elumelu watakuwa na msaada mkubwa sio tu Nigeria lakini bara nzima,” alisema.

Akizungumza kuhusu mchakato huo Ofisa Mtendaji Mkuu ajaye Ifeyinwa Ugochukwu, alisema “Programu ya Ujasiriamali wa Taasisi ya Tony Elumelu, imewawezesha kwa mafanikio wajasiriamali 7,520 katika miaka yake mitano ya kwanza kati ya miaka 10 ya programu. Ikitimiza miaka mitano kati ya miaka 10 ya programu, uteuzi wa mwaka huu umehusisha wajasiriamali 2,050
wakisaidiwa na washirika wa Taasisi.

“Mwaka jana, tulizindua TEFConnect - jukwaa la mitandao ya digital kwa wajasiriamali wa Kiafrika na kufunguliwa kwa wote - kuendeleza demokrasia ufikiaji wa fursa kwa maelfu ya wajasiriamali ambao hawawezi kufaidika moja kwa moja na Programu ya Wajasiriamali. Hii inaonyesha zaidi dhamira yetu yakuwawezesha wajasiriamali wetu na imani yetu kuwa ujasiriamali una ufunguo
wa kufuta uwezo wa kweli wa bara la Afrika,” alisema.

Alisema washirika wa taasisi hiyo kwa sasa wanazidi kuongezeka ni Kamati ya Kimataifa ya Msalaba Mwekundu (ICRC), United Nations Development Programme (UNDP), Serikali ya Benin (Seme City), Anambra State Government, Indorama,Serikali ya Botswana na Benki ya Maendeleo Afrika (AfDB).

Mwisho
Share To:

Post A Comment: