Wasanii
 maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Ali Kiba 
wamekutana katika msiba wa Agnes Masogange na kusalimiana.
Mara
 baada ya wasanii hao kusalimiana kwa kupeana mikono wakiwa katika meza 
kuu, waombolezaji waliojaa kwenye Viwanja vya Leaders walipiga kelele.
Diamond
 alimsalimia Kiba kwa kumpa mkono, kisha wawili hao walikumbatiana na 
baada ya tukio hilo, MC Pilipili alisikika akisema: “Unaona sasa, hawana
 ugomvi hawa.”
Kumekuwa
 na taarifa za wanamuziki hao kuwa na ugomvi kwa muda mrefu ambao hata 
hivyo, unatajwa kutengenezwa na mashabiki wao wa ‘Team Kiba na Team 
Diamond.’
Akizungumzia
 katika viwanja hivyo, Ali Kiba ambaye ametoka kuchukua jiko hivi 
karibuni, amesema harusi na kifo vyote ni ibada na ndiyo maana amefika 
kuungana na waombolezaji wengine ingawa bado yupo fungate.
Masogange alifariki dunia juzi katika Hospitali ya Mama Ngoma, Mwenge ambako alilazwa kwa siku nne.

Post A Comment: