Hali
 ni shwari mkoani Manyara. Hakuna dalili za maandamano. Hata hivyo 
askari polisi wakiwa na magari, pikipiki na kutembelea kwa miguu 
walionekana wakizunguka sehemu mbalimbali ili kuimarisha ulinzi. 
Kamanda
 wa Polisi wa Mkoa wa Manyara, Kamishna Msaidizi (ACP) Agustino Senga 
akizungumza  kwa njia ya simu  leo Aprili 26, amesema mkoa huo upo 
shwari kabisa. 
Kamanda Senga amesema polisi wapo kwenye maeneo tofauti ya mkoa huo wakiendelea na kazi ya ulinzi wa raia na mali zao. 
"Kwenye
 mkoa wangu hakuna mtu aliyeandamana wala aliyehamasisha mtu kuandamana 
wala hakuna aliyekamatwa juu ya hilo kwa kuhamasisha wala kuandamana," 
amesema kamanda Senga. 
Mkuu
 wa Wilaya ya Simanjiro, Mhandisi Zephania Chaula akizungumza juu ya 
maandamano hayo, aliwataka wananchi wenye nia hiyo kufanya shughuli zao 
za maendeleo na kuachana na suala hilo. 
"Kama
 kuna mtu ana hoja yoyote aje mezani tuzungumze juu ya hoja yake na siyo
 kutuletea habari za mambo ya kuandamana ambayo hayana tija yoyote kwa 
jamii," amesema Mhandisi Chaula. 

Post A Comment: