Kumekuwa na uvumi unaosambazwa katika mitandao ya kijamii kutoka kitengo cha Rais, Ikulu idara ya Mawasiliano ikidai kuwa, Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imearifu wananchi wake kufungia mitandao ya kijamii nchini endapo itatumika vibaya.

Kufuatia habari hiyo ambayo hata hivyo inaonesha ni ya mwaka 2017,  Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais- Ikulu, Gerson Msigwa mapema leo hii ameikanusha barua hiyo na kudai kuwa haijachapishwa na idara yake.

Msigwa amewasihi Watanzania kuipuuza habari hiyo kwani ni uvumi ambao hauna ukweli wowote, kwani Serikali haijatoa wala kuzungumzia swala hilo.

Share To:

msumbanews

Post A Comment: