Mwanamke mmoja kutoka nchini Marekani leo March 22, 2018 ameshikiliwa na polisi baada ya kusambaa kwa video kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha akimvutisha mtoto wake sigara.

Video hiyo ambayo iliangaliwa zaidi ya mara Milioni 1 ndiyo iliyofanya Polisi wajue kinachoendelea na kuanza kumtafuta mwanamke huyo anayejulikana kwa jina la Brianna Ashanti Lofton mwenye umri wa miaka 20.

Video hiyo ilimuonesha mama huyo akimpa mtoto sigara ili avute. Lofton ameshtakiwa pia na kosa na kukutwa na bangi na makosa mawili ya kunyanyasa mtoto.
Share To:

msumbanews

Post A Comment: