Waziri wa Habari,Utamaduni,Sanaa na Michezo  Nape Moses Nnauye ameahidi 
kutoa shilingi laki tano kwa kila goli litakalofungwa na timu ya 
Serengeti Boys  katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Kombe la 
mataifa ya Afrika kwa vijana chini ya umri wa miaka 17 utakaofanyika 
kesho katika Uwanja wa Taifa dhidi ya Congo-Brazzaville.
Akiongea
 na waandishi wa habari leo Jijini Dar es Salaam Nape amesema milango 
ipo wazi kwa wadau wengine wa michezo kujitolea katika kuiwezesha timu  
na hivyo kufanya vizuri katika  mechi hii ambayo ni muhimu sana kushinda
 ili kufuzu kwa fainali hizo.
“Hii timu ni yetu sote hivyo 
inahitajika tuimiliki, tuepe nguvu, tuiombee ili iweze kufanya vizuri na
 hatimaye kufuzu kuingia fainali kwa kuitoa timu ya Congo-Brazzaville” 
amesema  Nape.
Ameongeza kuwa kesho asubuhi atakutana na 
wachezaji wa timu hiyo ili kuwapa maneno ya faraja kabla ya kuanza kwa 
mechi na kuwataka watanzania  kujitokeza kwa wingi uwanjani ili kuwapa 
motisha wachezaji kwa kuwashangilia  na kuwatia moyo.
Mbali na 
hayo Waziri Nape ametoa ufafanuzi kuhusu matumizi ya kadi za 
kieletroniki zilizozinduliwa hivi karibuni kwa kueleza kuwa kadi hizo 
bado hazijaanza kutumika rasmi ili zitaanza kutumiwa katika mchezo baina
 ya Wabunge wa Simba na Yanga pamoja na Bongo Fleva.
Timu ya Serengeti Boys inaundwa na vijana wa Kitanzania wenye umri chini ya miaka 17 ambapo katika mchezo wa kesho watahitaji ushindi na baadaye kufanya mechi ya marudiano mnamo Oktoba 2 mwaka huu nchini Congo-Brazzaville.
www.msumbanews.blogspot.com



Post A Comment: