Mwanamuziki Beyonce ameahirisha tamasha lake la New Jersey kwa jina World Tour baada ya madaktari kumshauri kupumzisha sauti yake.


Msanii huyo ambaye alisheherekea siku yake ya 35 ya kuzaliwa siku ya Jumapili alitoa taarifa akisema tamasha hilo halitafanyika mnamo tarehe 7 mwezi Octoba.
Hatahivyo ataendelea na tamasha nyengine katika miji ya Los Angeles,Houston,New Orleans na Atlanta kama ilivyopangwa.
Ziara hiyo ambayo inalenga kuuza albamu yake mpya Lemonade,ilianza mjini Miami mnamo tarehe 27 mwezi Aprili.
Ilitarajiwa kukamilika Nashvile mnamo tarehe 2 mwezi Octoba,lakini sasa inaonekana kwamba New Jersey itaanda tamasha lake la mwisho
Share To:

msumbanews

Post A Comment: