Mkuu wa mkoa wa Iringa akiongea na wananchi mara baada ya kukabidhiwa vyumba vya madarasa na mkuu wa wilaya ya Iringa
Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga akikagua vyumba vya madarasa akiwa sambamba na mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo,mwenyekiti wa Halmashauri ya Iringa Stephen Mhapa mara baada ya kukabidhiwa vyumba ambavyo vimekamili kwa asilimia 100
Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Bashir Mhoja akiwaonyesha ubora wa vyumba vya madarasa Mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga na mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo
Na Fredy Mgunda,Iringa.
MKUU
wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo ameishukuru serikali kwa kutatua
changamoto ya vyumba vya madarasa ambayo yatasaidia wanafunzi wote
waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza kupata nafasi katika mwaka huu wa
masomo.
Amezungumza
hayo wakati wa kukabidhi vyumba vya madarasa 94 mkuu wa mkoa wa Iringa ambavyo
vimejengwa kupitia mradi wa 5441 TCRP ambavyo vyumba vya madarasa ya sekondari
66 na shule shikizi 28 katika Halmashauri ya wilaya ya Iringa.
Moyo
alisema kuwa anampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa
Samia Suhulu Hassan kwa namna ambavyo amefanikiwa kupambana na ugonjwa wa UVIKO
19 na kufanikiwa kupata mkopo wenye masharti nafuu kutoka Shirika la Fedha
Duniani (IMF) wa kiasi cha shilingi Trilioni 1.3 kwa ajili ya kusaidia kufufua
uchumi katika sekta ambazo zimeathirika kutokana na janga.
Alisema
kuwa Halmashauri ya wilaya ya Iringa ilipokea kiasi zaidi ya shilingi Bilioni
mbili kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa ya sekondari 66,shule shikizi 28
na nyumba za walimu kwa ajili ya maendeleo ya kukuza sekta ya elimu pamoja na
ujenzi wa wodi katika sekta ya afya.
Moyo
alisema kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa hayo ulianza mwanzoni mwa mwezi wa
kumi na moja mwaka 2021 na kukamili kabla ya tarehe saba mwezi wa kwanza mwaka
2022.
Alisema kuwa ujenzi wa vyumba hivyo vya
madarasa umekuja kutokana na idadi ya wanafunzi ambao watajiunga kuanzia mwenzi
wa kwanza mwaka huu 2022 ambapo inajumuisha viti na madawati.
Aidha
moyo alisema kuwa hakuna mwanafunzi atakayekosa sehemu ya kukaa akiwa amechaguliwa
kujiunga kidato cha kwanza katika shule yeyote ilivyopo katika Halmashauri ya
wilaya ya Iringa na kuwahimiza wazazi kuwapeleka shule wanafunzi wote
waliochaguliwa kuingia kidato cha kwanza.
Moyo
aliongeza kuwa lengo la kujenga vyumba vya madarasa 28 vya shule shikizi ni
kuwapunguzia adha wanafunzi wanaotoka mbali na maeneo ambayo shule mama ipo ili
nao waweze kupata elimu iliyo bora kama wanafunzi wengine.
Alisema
kuwa hadi kufikia siku ya tarehe sita mwezi wa kwanza mwaka 2022 wamefikia
asilimia 99 ya ujunze wa vyumba vyote vya madarasa ambavyo walitakiwa kujenga
kutokana na fedha hizo za mkopo nafuu kutoka IMF.
Moyo
alimalizia kwa kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa
Samia Suluhu Hassan kwa kuipatia fedha hizo ambazo zimesaidia kutatua
changamoto hiyo ambavyo ilikuwa inawakabiri wananchi na kuongeza ajira za muda
kwa wale waliokuwa wanafanya kazi ya ujenzi wa vyumba hivyo vya madarasa hayo.
Kwa
upande wake mkuu wa mkoa wa Iringa Queen Sendiga alisema ujenzi wa vyumba vya
madarasa 94 sio jambo rahisi kwa Halmashauri hivyo ameupongeza uongozi wa
halmashuri hiyo kwa kazi kubwa ya kusimamia ujenzi huo kukamilika kwa wakati.
“Alinipigia
simu baba yangu na kuniuliza kuwa wewe mtoto wangu kwenye mkoa wako unajenga
madarasa mangapi? Nikamjibu kuwa nina madarasa akasema kuwa huyo binti yangu Samia kazi
aliyoifanya haijawahi kufanywa na kiongozi yeyote Yule toka apate akiri na
ilikuwa inachukua miaka mnne kupata darasa moja ili watoto waweze kusoma ndio
maana watoto wengi walikuwa wanashindwa kuendelea na masomo” alisema RC Sendiga
Sendiga
alisema kuwa jitihada hizo ni maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan ambayo hayajawahi kufanywa na kiongozi mkubwa
kaka yeye ndio maana ameweka history ya kipekee.
Alisema
kuwa miaka ya nyuma ilikuwa ikifika kipindi kama hiki wazazi wengi hukimbia
makazi yao kutokana na kukimbia majukumu ya kuchangia ujenzi wa madarasa na
elimu ya watoto wao na wazazi wengine hulazimika kuuza mali zao ili kumudu
kugharamia elimu ya watoto.
Sendiga
alisema kuwa watanzania wanatakiwa kuendelea kumuunga mkono Rais wa Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa jitihada zake
anazozifanya za kuleta maendeleo ya nchi.
Aidha
Sendiga alisema kuwa miradi yote aliyoitembelea siku ya leo imekuwa miradi bora
na yenye viwango ambavyo vinatakiwa hivyo aliwapongeza uongozi wa Halmashauri
ya wilaya ya Iringa kwa kusimamia vilivyo miradi hiyo ya kimaendeleo.
Aliwataka
wazazi kuwapeleka shule watoto wenye mahitaji maalumu kwa kuwa serikani tayari
imepokea fedha kwa ajili ya ujenzi wa mabweni mawili kwa ajili ya wanafunzi
wenye mahitaji maalum hivyo wazazi hawapaswi kabisa kuwafungia watoto hao
badala yake wanatakiwa kuwapeleka shule.
Alisema
katika miradi ya maji ambayo ameikagua kwa kiasi kikubwa imemlizisha kwa namna
ambavyo imetekelezwa na kuhakikisha inamtua ndoo mwanamke kama ambavyo Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan anayotaka.
Kwa
upande wake mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Iringa Stephen Mhapa alisema
kuwa watumishi wamefanya kazi kubwa kuhakikisha kila mradi unatekelezwa kwenye
Halmashauri hiyo unatekelezwa kwa wakati na ubora unatakiwa kulingana na
thamani ya fedha iliyotolewa kwa ajili ya mradi.
Mhapa
alisema kuwa kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongozi wa serikali wamekuwa
wakiwakatisha tama watumishi hao kwa kuongea maneno magumu tofauti na uhalisia
wa kazi ambazo wanazitekeleza.
Post A Comment: