Mwenyekiti wa CCM mkoani Iringa Dr. Abel Nyamahanga,Meneja wa TARURA Wilaya ya Iringa Barnaba Selemani Jabir na mkuu wa wilaya ya Iringa Mohamed Hassan Moyo wakiwa wanapita kwenye daraja lililosimamiwa na TARURA wilaya ya Iringa
Mbunge wa jimbo la Kalenga Jackson Kiswaga akipita kwenye daraja ambalo limesimamiwa na TARURA wilaya ya Iringa likiwa na ubora ambao hata mbunge huyo amefurahishwa nalo
Meneja wa TARURA Wilaya ya Iringa Barnaba Selemani Jabir akiwa na mwenyekiti wa umoja wa vijana wilaya ya Iringa Makala Mapesah na mwenyekiti wa wazazi CCM mkoa
Na Fredy Mgunda,Iringa.
CHAMA cha mapinduzi Mkoa
wa Iringa kimesema wakala wa barabara TARURA Wilayani Iringa imetekeleza kwa
vitendo dhamira ya Serikali ya kuharakisha maendeleo kwa wananchi kwa
kufanikiwa kutekeleza miradi yao kwa wakati
Akizungumza wakati wa
ziara ya kamati ya Siasa ya chama cha mapinduzi Mkoa wa Iringa (CCM) ya ukaguzi
wa miradi ya maendeleo, Mwenyekiti wa CCM mkoani Iringa Dr. Abel Nyamahanga
akiongoza katika ziara ya amesema wameridhishwa na TARURA hasa kwa kufanikisha
ujenzi wa daraja la Ifunda.
Dr. Nyamahanga alisema
kuwa kamati ya siasa ya mkoa wa Iringa inapongeza na kueleza kuridhishwa na namna
ambavyo TARURA wanavyotekeleza miradi yao huku akisisitiza kuwa mradi wa ujenzi
wa barabara Na daraja la Ifunda Bandabichi kuwa utaleta mapinduzi ya kiuchumi
kwa jamii
Alisema TARURA Wilayani
Iringa wamefanikiwa kutekeleza kwa vitendo azma ya serikali ya awamu ya sita
katika kuchochea maendeleo ya haraka kwa wananchi huku akiwahimiza wananchi
kuitunza miundombinu hiyo
Lakini pia Dr. Nyamahanga
aliipongeza serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania inayongozwa na Rais wa
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan kwa kutoa fedha
nyingi mkoa wa Iringa kwa ajiri ya maendeleo ya ujenzi wa barabara na madaraja
mkoni humo
Kiongozi huyo wa CCM mkoa
wa Iringa wakati wa ziara hiyo amepokea taarifa ya maendeleo ya ujenzi wa
barabara Na daraja la Ifunda Bandabichi, huku akisema kuwa daraja hilo ni
mkombozi wa Kiuchumi kwa wananchi wa maeneo hayo
Kwa upande wake Meneja wa
TARURA Wilaya ya Iringa Barnaba Selemani Jabir aliyebainisha gharama za mradi
wa ujenzi wa barabara ya Ifunda Itengulinyi pamoja na madaraja mawili moja
likiwa ni watembea kwa miguu umegharimu kiasi milioni 984
Kukamilika kwa mradi huo
kunatajwa kuwanufaisha wakazi wa takribani kata tano ikiwemo Kata ya Ifunda,
Lumuli, Maboga, wasa na Tungamalenga za wilayani huo.
Meneja wa TARURA Barnaba
Selemani Jabir ameipongeza na kuishukuru Serikali kwa kuboresha bajeti ya
TARURA na kuitaja kuwa na tija kwa wilaya
Vumilia mwenda diwani wa
viti maalum Tarafa ya Kiponzero ameeleza maswahibu yaliyokuwa yakiwakabili
waananchi waliokuwa wakilazimika kuvuka mto uliopo eneo hilo kabla ya ujenzi wa
daraja.
Alisema kabla ya ujenzi
wa barabara hiyo wananchi wengi walikuwa wanalazimika kuvua nguo kwanza ili
waweze kuvunga mto huo hivyo ujenzi wa daraja hilo umekuwa mkombozi kwa
wananchi wa zaidi ya kata tano ambao wanatumia kupita katika barabara hiyo.
Post A Comment: